Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Malaika

Malaika ni nani ?

Biblia inasema nini? Kabala ya mungu kuumba ulimwengu na wanadamu, tayari alikuwa ameumba viumbe wenye akili sana kuliko wanadamu.

Wana nguvu nyingi kuliko wanadamu, nao wanaishi mbinguni pamoja na mungu, mahali ambapo wanadamu hawawezi kuingia au kupaona. ( ayubu 38: 4,7 ) ktk Biblia, viumbe hao wenye uwezo mkubwa wanaitwa " roho " au " malaika " zaburi 104:4

( Biblia husema kwamba baadhi ya viumbe wa roho waliasi mamlaka ya mungu, na malaika hao wabaya wanitwa " roho waovu " Luka 10:17,20 )

Kuna malaika wangapi? Wengi sana.
Malaika wanaokizunguka kiti cha enzi cha mungu ni " makumi ya maelfu ya makumi ya maelfu na maelfu ya maelfu " ( Ufunuo 5:11 ) Ikiwa usemi huo si wa mfano, basi kuna mamia ya mamilioni ya malaika

" Nami nikaona .... Malaika engi kuzunguka kile kiti cha ufalme..... Na hesabu yao ilikuwa makumi ya maelfu ya makumk ya maelfu na maelfu ya maelfu. " - ufunuo 5:11

Malaika ni jeshi la mungu wanaoishi na mungu mbinguni wakifanya kazi za mungu pamoja na wana wa mungu yani binadamu hapa duniani.

Ukweli sio rahisi kumuona malaika wa mungu kwa macho yetu haya ya nyama bali tunaishi nao kwa imani, kwa kuamini tu, maana maandiko yanasema hivi " Tunalindwa na nguvu za mungu kwa njia ya imani "

Wanatenda kazi zao na kuwalinda watu wanotembea na neno la mungu je unataka kulindwa na malaika?

Basi tembea na neno la mungu kwa maana malaika hawa wanasikia neno la mungu wala sio neno lako wewe mwanadamu.

Wako haina mbili za malaika

1: malaika w nuru
2: malaika wa giza

Malaika wa giza
Malaika wa giza ndio mashetani ni wahasi, walihasi neno pamoja na mamlaka za ufalme

Malaika hawa ni wakolofi ndio wanaoleta magonjwa kwenye familia, kifo, vita, njaa nk

Wanachuki dhidi ya mungu na ufalme wake na wanawake pia.

Hawapendi kuona maendeleo ya wana hawapendi kabisa.
Makao yao makubwa ni kuzimi.

Pia malaika hawa wanapatikana kwa waganga wa kienyeji kwa wachawi, wasoma nyota, madabii wa uwongo huku ndiko wanapo kaa kwa watumishi wao.

Kwa leo tunaishia hapa asante sana rafiki usikose makala yeyote hapa hapa msikivublog karibu tena juma lijalo



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...