Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Chanzo cha Ganzi na kuchomwa na pini mwilini

Mojabya maswali ninayoulizwa na kulalmikiwa sana na watu wenye umri mkubwa ni uwepi wa ganzi na hisia za kuchoma na kama pini miguuni.

Ingawa dalili hizi zinaweza kutokea kokote pale mwilini ikiwemo mikononi, vidoleni, mabegani.
Kuna sababu nyingi za kujitokeza kwa hali hii ikiwamo pale unaposimama au kukaa mahali pamoja muda mrefu.
Majeraha ya shingo au pingiri za mgongo yanaweza kusababisha ganzi na kuchomachoma ktk mabega na mgongo.
Kama mtu atakuwa na majeraha ktk mgongo au kiuno anaweza pia kupata ganzi ktk maeneo ya miguuni.
Uwepo wa mgandamizo unaoleta shinikizo ktk mishipa ya fahamu inayotokea ktk uti wa mgongo mfano santuri za mgongo zinapi choropoka.
Shinikizo ktk mishipa ya fahamu baada ya kugandamizwa na mshipa ya damu uliotuna, uvimbe, kovu la tishu na uwepo wa uambukizi yote yanasababisha ganzi.
Maambukizo ya virusi vya mkanda wa jeshi, damu kuwa chache au kutofikia sehemu fulani mwili ikiwamo kujeruhiwa na theluji au mishipa ya damu kuharibika.
Kuwa na kiwango kisicho cha kawaida cha madini mbalimbali ikiwamo kalsiumu, potasiamu na sodiamu.
Ukosefu wa vitamini B na viatamini nyingine pamoja na virutubisho mbalimbali mwilini pia ni mojawapo ya ganzi mwilini .
Pia matumizi ya dawa za matibabu ikiwamo dawa za kifua kikuu ( TB ) na kufubaza makali ya VVU huambatana na hali hii.
Matibabu ya mionzi nayo yanambatana na kujitokeza kwa ganzi mwilini.
Vitu kama madini ya risasi, pombe na kemikali tiba za kutibu saratani huweza kusababisha ganzi mwilini kwani zina haribu mishipa ya fahamu.
Kuumwa na wadudu au wanyama ikiwamo nyoka, buibui, nge na aina ya mijusi wakubwa na jamii ya viumbe wa baharini pia kunaweza kuleta ganzi.
Maradhi ni kama vile kisukari, kipanda uso, ugonjwa wa kinga, kifafa nk
Asante sana juma lijalosuluhisho la ganzi hapa msikivu blog

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...