Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Vijidudu na Namna ya kuviepuka na kuviua

Vijidudu, yaani bacteria, ni vidogo mno navyo havionekani kwa macho matupu, ila kwa darubini tu, lakini vina uhai, hujilisha na kujiongeza kwa upesi sana. vijidudu hivi vyapatikana po pote ktk vumbi, takataka, udongo, mimea na chakula.
Vimo vile vile ktk ngozi yetu na ya wanyama, hata ktk ngozi ile nyororo.
Vimo kinywani, kooni mpaka tumboni kuyeyusha chakula navyo hutoka pamoja na kinyesi.
Lakini havipatikani ktk viungo vingine vilivyofunikwa kama vile musuli, moyo, maini, mishipa ya damu na kadhalika.
Kabisa havipatikani ktk kibofu au ktk mji wa mimba wala ndani ya mimba.
Vijidudu vyo vyote vile viingiapo ktk viungo hivyo huviharibu kabisa.
Basi tuangalie sana tusiingize vijidudu hivyo ktk viungo kutoka ktk ngozi au ktk kinyesi, sababu ingawa vitaingia vijidudu huitwa kiungo safi kabisa ( sterile )
Ktk vijidudu vile vyenye maana yaani viyeyushavyo chakula tumboni hivi hudhuru sana vikiingia ktk viungo vinginevyo.
Vile vile tukiingiza mrija wa kutolea mkojo ktk kibofu na hivyo hudhuru sana; yaani baada ya siku chache hutokea ugonjwa wa kibofu uitwao kwa kiganga Cystist.
Vivyo hivyo tumpimapo mzazi wakati wa kuzaa au wakati wa kutoa kondo kwa mikono au vyombo visivyo safi kabisa basi twamwambukiza vijidudu.
Kuambukiza hakuonekani Mara kwa kuwa vijidudu hutuia siku au muda fulani mpaka vimejizidisha na kuwa vingi vya kutosha na kutoa maradhi.
Muda huo huitwa muda wa kujizidisha ( the incubation period ) lakini muda huo watofautika kwa kila maradhi, kwa kawaida huchukua siku chache tu.

Vijidudu viletavyo maradhi vyapangika hasa ktk aina nne:

1:  Cocci vyenye sura ya vinukta.

2:  Bacilli vyenye sura ya vistari

3:  Spiroketi vyenye sura ya vijinywele vilivyopindana.

4:  Vires ni vijidudu vya maumbile ya pekee vidogo sana kuliko bacilli na havionekani kwa darubini ya kawaida.

Aina yo yote ya vijidudu akiambukizwa nayo mama mzazi huugua sana.
Habari hizi zote hazijuliwi na wakunga wenyeji wasiojua ku soma.
Wao hueleza ajali mbaya kuwa ni matokeo ya kulogwa, ama adhabu ya kuvunja mwiko na kdhlika.
Hivyo huwa hawafaulu ktk uzazi wenye taabu na shida hasa waingizapo mikono michafu ukeni au ktk mji wa uzazi.
Ni dhahiri wazazi huuawa na wakunga wenyeji ingawa huwa na nia njema ya kusaidia.

Njia za kuua vijidudu

Yajulikana kuwa hakuna vujidudu viwezavyo kuishi muda mrefu ndani ya maji ya kuchemka au mvuke wake.
Kwa hiyo twafahamu kuwa vyombo vyote vitumikavyo ktk ukunga visivyodhurika na maji ya moto lazima vichemshwe ktk maji u mvuke wake.

1. Vyombo vya madini kama vile koleo, vibano na sahani na kadhalika, hivi vyote vitiwe ndani ya maji ya kuchemka kwa muda wa dakika 20. Kuhifadhi makali ya visu yafaa kuvifunika na pamba tena vitiwe ndani ya alcohol.

2. Vyombo vyote vya mpira vichemshwe vile vile lakini kwa muda wa dakika 5 tu. Baadaye vifunikwe na kitambaa safi kabisa, au tunaweza kuvitia ktk boz la chuma lililifungwa kabisa pamoja na tunaweza kuvitia ktk box la chuma lililofungwa kabisa pamoja na vodonge vya Formalin kwa muda wa saa 24.
Vyombo vya namna ya bilauri kama vile bomba la sindano, kitilio vichemshwe vile vile muda wa dakika 20.
Lakini tuangalie kuvitia ndani ya maji kabla hayajachemka na vifunikwe na kitambaa

3. Nguo na vitambaa vya kufungia ( dressings ) lazima vichemshwe ktk sufuria ipitishayo mvuke kwa nguvu ( sterilizer ) humo muda wake ni mfupi kama dakika 20 tu.
Kama hakuna sterilizer unaweza kuvichemsha vitambaa ktk sufuria na baadaye kuvinyosha na pasi.
Hii siyo safi kabisa ( sterile ) lakini ni safi.
Vyombo vyote viharibiwavyo na maji ya kuchemka, hivi hufanywa safi kabisa vikitiwa ndani ya dawa zinazoua vijidudu ziitwazo Dawa hizo ni lotions

a.  Lysol, sehemu moja kwa mia ( 1% )

b. Dettol 1%

c. Cetavolon, sehemu moja kwa mia ( 1% )
Namna ya kunawa mikono na ngozi viwe safi kabisa ( sterile )

1.  Mikono : yatumika dakika kumi. Pete, bangili zinavuliwe, kucha zikatwe na kusafishwa sana.

a:  Tunawe mikono kwa maji na sabuni muda wa dakika saba na pasipo kufuta tuitie

b:  Ndani ya lotion ya Dettol 1/2% au ndani ya Lysol 1/2% au Cetavlon 1/2% Kwa muda wa dakika tatu. Kila tukichafuka, mfano, kwa kushika kitu au kiungo kisicho safi kabisa, yatulazimu tuioshe mikono yetu tena ndani ya lotion muda wa dakika chache.

2.  Ngozi ya mzazi: Isafishwe kwa kitambaa laini ( gauze ) kilichochovywa ktk lotion yo yote, tupanguse mbele ( vulva ) mara tatu toka juu kwenda chini na kila mara tukitupe kitambaa anapasuiwa ( Operation ) ngozi ya juu ipakwe Tr of lodine sehemu 2,5 kwa mia ( 2,5% ) au mercurochron 1% au disinfectants nyinginezo

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...