Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mtafiti aliyezalisha mbegu bora ya mpunga

Unamfahamu mtafiti mwanamke aliyewezesha nchi kupata mbegu bora za mpunga ili kukabiliana na uharibifu wa udongo?
Kituo cha utafiti wa kilimo cha chollima kilichoko, Dakawa, Morogoro kimeleta mafanikio kupitia utafiti uliofanywa na mkuu wa kituo hicho, Dk sophia Kashenge Kilenga ambaye anaongoza jopo la watafiti wa mbegu bora za mpunga.
Mtaalamu huyo aliyefanikisha kituo hicho aliyefanikisha kituo hicho kuzalisha mbegu bora zinazoweza kukabiliana na uharibifu wa udongo ktk mashamba ya umwagiliaji ya mpunga yanayokabiliwa na ongezeko la chumvi.
Mbegu za mpunga tatu ambazo mtafiti huyo amezalisha ni SATO1, SATO6 na SATO9 ambazo ni bora zaidi kukabiliani na ongezeko la chumvi ktk mashamba ya umwagiliaji mpunga.
" Mbegu moja kati ya hizo tatu, SATO1 ilidhinishwa na kamati maalumu ya mbegu iliyoko wizarani machi 18 2016"

Anasema utafiti kuwa:

" Kila mbegu ina uwezo wake wa kukua kulingana na aina ya udongo "

Anaendelea kueleza kuwa ili kuboresha utafiti huo, mwaka 2013 alianzisha mradi mwingine wa utafiti chini ya mpango wa shirika la msaada la maendeleo la kimataifa marekani

( Usaid ) iAGRI Kwa ajili ya kutafiti njia bora ya kubadili mfumo wa ardhi ktk nashamba ya umwagiliaji mpunga ya ndugu ya wilayani same, Mkoa wa kilimanjaro.
Ktk maboresho hayo ya utafiti, alisema watafiti walibaini matumizi ya madini ya Gypsum, mboji na taka zitokanazo na mabaki ya mbo zikiwekwa ardhi isiyorutubishwa.

" Matokeo haya ya utafiti wa muda mrefu ni muhimu sana kwa kuwa ongezeko la chumvi ni chachu inayoua udongo taratibu.
Kupatikana kwa tiba hii kutasaidia sana kuongeza mapato ya wakulima wa mpunga kwani chumvi imekuwa ikisababisha kupunguza kwa mapato, "
Anasema.
Matokeo ya utafiti huu pia yatasaidia wakulima wadogo wengi wa mpunga ambao wanakabiliana na umaskini.
Matokeo haya ya utafiti ni ufumbuzi wa kuongeza mapato ktk uchumi wa familia na taifa kwa ujumla kwani usalama wa chakula pia utaimarika

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...