Miaka michache iliyopita, watafiti waliripoti kugunduliwa kwa mimea fulani inayoota chini ya maji, wanayoamini imeishi kwa maelfu ya miaka, huenda muda mrefu kuliko kiumbe kingine chochote duniani.
Mimea hiyo ni ya jamii ya posidonia oceanica, aina fulani ya nyasi zilizoenea kwenye sakafu ya bahari ya Mediterania kati ya Hispania na saiprasi.
Ikiwa mimea inaweza kuishi kwa miaka mingi hivyo, namna gani wanadamu? Baadhi ya wanasayansi ambao huchunguza suala la uzee wanahisi kwamba kuna uwezekano wa kuongeza muda wa kuishi. Kwa mfano, kitabu fulani kuhusu suala la uzee kinasema kuwa kinachunguza kwa kina " maendeleo makubwa ya kisayansi " ktk nyanja hiyo.
Hatujui ikiwa maendeleo ya kisayansi yatakuwa na mchango wowote ktk kuongeza muda wa kuishi wa mwanadamu au la.
Hata hivyo, tumaini la kweli la kuishi milele halitegemei sayansi.
Biblia inatueleza kwa muumba wetu, yehova mungu, na kusema hivi: " kwako wewe iko chemchemi ya uzima" ( zaburi 36:9 ) yesu kristo alisali hivi kwa mungu:
" uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, yesu kristo." ( yohana 17:3 ) kwa kweli, jitihada zetu za kumjua na kumpendeza yehova mungu na mwana wake, yesu kristo, zitathawbishwa kw baraka za milele
Asante sana ndugu kwa leo tunaishia hapa.
Maoni
Chapisha Maoni