Ruka hadi kwenye maudhui makuu

WAFU WAKO WAPI Na Wilson mtishbi

Kwa ufupisho, Biblia inasema kwamba wafu wako kaburini wakingojea ufufuo. ( yohana 5: 28, 29 ) inasema hivi "Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja,ambayo watu wote waliomo makaburini watasikia sauti yake Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu." Hawateseki au kuhisi maumivu yoyote, kwa sababu " wafu, hawajui lolote kamwe." ( mhubiri 9: 5 ) inasema hivi "kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lolote , wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahuliwa." katika mafundisho yake, Yesu alilinganisha kifo na usingizi mzito. ( yohana 11: 11- 14 ) Hivyo basi, Hatuna sababu yoyote ya kuwaogopa wale waliokufa au kuwatuliza kwa kuwatolea vitu mbalimbali. Hawawezi kutusaidia wala kutudhuru, kwa sababu " Hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi wala hekima ktk kaburi." ( Mhubiri 9: 10 ) Hata hivyo, kupitia ufufuo, Mungu atakishinsa kifo milele. ( 1 wakorintho 15: 26 ) inasema hivi " Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti na 55 inasema hivi " Ku wapi, Ewe mauti, Uchungu wako

HAKUNA ANDIKO KATIKA BIBLIA LINALOTAJA KUHUSU " NAFSI ISIYOWEZA KUFA"
Ki ya kati, Wanafalsafa Wagiriki walikuwa wameeneza fundisho hilo, na muda mfupi baadaye, lilienea ktk Milki yote ya Ugiriki. Katika karne ya kwanza W. K ., Madhehebu mawili maarufu ya kiyahudi, ambayo ni waesene na mafarisayo, yalifundisha kwamba nafsi huendelea kuishi baada ya mwili kufa . kitabu The jewish Encyclopedia Kinasema : " Fundisho la kutokufa kwa nafsi liliwafikia Wayahudi baada ya kuanza kupokea mawazo ya Wagiriki hasa kupitia falsafa ya Plato." Vivyo hivyo, Josephus, mwanahistoria Myahudi wa karne ya kwanza alisema fundisho hilo halitokani na maandiko matakatifu, bali linatokana na " imani ya wana wa Ugiriki ", Aliyoiona kuwa mkusanyo wa hekayo zao. Kadiri tamaduni za Wagiriki zilivyoenea, watu waliodai kuwa Wakristo walianza pia kukubali fundiaho hilo la kipagani. Kulingana na mwanahistoria Jona Lendering, " Ilikuwa rahisi kuunganisha falsafa ya Plato kwamba mwanzoni nafsi zetu zilikuwa mahali pazuri na sasa zinaishi ulimwengu uliopotoka." Hivyo, fundisho la kipagani kuhusu kutokufa kwa nafsi likapenya katika kanisa la " kikristo " na kuwa sehemu kuu ya imani yake.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...