Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Somo : Roho Mtakatifu part 2 Na Mwl Christopher Mwakasege

Kijiti kilichowaka moto ili mungu apate utayari na usikivu wa moyo wa musa ktk kile alichotaka kuzungumza naye wakati ule

Musa alikuwa anaendelea na kazi ya kuchunga kundi la kondoo la baba mkwe wake wakati alipoona mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti akatazama na kumbe kile kijiti kiliwaka moto nacho kijiti hakikuteketea ( kutoka 3:2 )
Ukiifatilia habari hii kwa makini utaona ya kuwa mungu hakujifunua na kusemabna musa hadi musa alipogeuka kutoka kujua kwa nini kijiti hakiteketei, ingawa kilikuwa kinawaka moto na musa alipogeuka na Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti akasema musa musa akasema mimi hapa ( kutoka 3:4 ) mungu lizungumza mambo kadha wa kadha kabla musa hajakubali kuupokea na kuutekeleza wito aliyoitiwa, utayapata mambo hayo ( kutoka 3,4,22 ) na ( kutoka 4,1,29 )
Ninachotaka tujifunze hapa si ile hatua ya mungu ya kujifunua na kusema na musa Ninachotaka tujifunze katika habari hii ni kutoka kujua juu ya sababu iliyomfanya mungu ajifunue jinsi alivyojifunua yaani ya kutumia moto, sababu hiyo tunaipata tunaposoma maneno ambayo mungu alisema na musa mara tu baada ya musa kuitika alipoitwa jina lake Biblia inatueleza maneno ambayo mungu aliyasema kutoka katikati ya kijiti kilichokuwa kinawaka moto lakini bila kuteketea mungu alimwambia musa hii usikaribie hapa vua viatu vya miguuni mwako maana mahali hapa unaposimama ni nchi takatifu ( kutoka 3:5 )
Mungu alikuwa ana maana gani alipomwambia musa hivi vua viatu vyako miguuni mwako kufuatana na ( waefeso 6: ) miguu huwa inabebeshwa jukumu la kuchukua utayari wa kutumwa kupeleka habari muhimu mahali inapotakiwa kupelekwa wakati ule mungu alipotakiwa kupelekwa wakati ule mungu alipokuwa anazungumza na musa miguu ya musa ilikuwa imebebaa utayari wa kutumwa na baba mkwe wake aliyeitwa yethro kwenda kuchunga kundi lake la mifugo na inaonekana wazi ya kuwa mungu aliona ya kuwa viatu alivyovaa musa au utayari aliokuwa nao musa wa kumsikiliza Baba mkwe wake kwa wakati ule usingempa usikivu wa kutosha wa kusikiliza kile ambacho mungu alitaka kusema naye
Mungu hakujifunua kwa musa wala kumpa maelekezo yaliyohusu wito wake hadi musa alipovua viatu vyake kwa hiyo tunaweza kusema mungu alijifunua kwa kutumia moto kwenye kijiti ili apte utayari na usikivu wa moyo wa musa ktk kile alichotaka kuzungumza naye wakati ule kumbuka Agano la kale lilifungwa kwa mwili au kwa mtu kutahiriwa kwa jinsi ya mwili lakini Agano jipya lilifungwa na linafungwa kwa mtu kutahiriwa moyo wake kwa jinsi ya rohoni kwa mantiki hii ina maana ktk agano jipya moto wa roho mtakatifu ambao mungu atatuweka miyoni mwetu wakati anataka mioyo yetu iwe na utayari na usikivu kwake kwa hiyo wakati mwingine unaposikia moto unawaka moyoni mwako Bila kuzimika ujue kuna uwezokano mkubwa kuwa mungu anatafuta utayari na usikivu wa moyo wako ktk kile anachotaka kukueleza moto kwenye kijiti uliambatana na kile ambacho mungu alitaka asikie lakini baada ya musa kugeuka na kuitika kwa hiyo unaposikia moto moyoni mwako mwambie mungu kwa njia maombi ya kuwa umegeuka na uko tayari kumsikiliza naamini mungu atakusemesha kile alichotaka usikie kutoka kwake

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...