Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Roho Mtakatifu part 7 Na Mwl Christopher mwakasege

Roho Mtakatifu anataka ufahamu na ujue mambo gani ikiwa nakupa kukujulisha juu ya ukiwa kuwepo ktk eneo.

Biblia inasema ktk ( mwanzo 1:2 ) hivi nayo nchi ilikuwa ukiwa na roho ya mungu ikatulia juu ya uso wa maji kufuatana na neno nchi lilivyotumika hapa lina maana ya ardhi.

Hii ni kwa kuwa tafsiri nyingi za Biblia za uingereza zimetumia neno earth pamoja na kwamba ardhi hiyo ilikuwa chini ya maji au ilikuwa imefunikwa na maji.

Roho Mtakatifu aliweza kujua hali ya ukiwa iliyo kuwa kwenye ardhi ya eneo lile na tunaposoma ( Ezekiel 15:8 )

Tunajua ya kuwa ukiwa ni matokeo ya adhabu ya mungu mstari huu umeandikwa hivi nami nitaifanya nchi kuwa ukiwa kwa sababu wamekosa asema Bwana mungu mstari huu unatupa kujua jambo muhimu ya kwamba ukiwa unaweza ukakaa juu ya ardhi au ktk ardhi ya eneo hata kama eneo hilo la ardhi au ktk ardhi ya eneo hata kama eneo hilo la ardhi halina watu wakati huo

Je hali ya namna hii unapoisikia moyoni mwako UNAPOOMBEA eneo la ardhi unayotaka kununua kwa ajili ya kujenga nyumba au kuitumia kwa kilimo Roho Mtakatifu anataka kukupa ujumbe gani ??

Ikikutokea hali ya namna hiyo ujue Roho Mtakatifu anataka ufahamu ya kuwa

__  Eneo hilo lipo chini ya adhabu ya mungu

__  Kuna kosa lililofanywa na mtu au watu waliokaa au waliomiliki eneo hilo kabla yako

__  Kwamba kosa hilo linatakiwa lirekebishwe kwa toba kabla mtu mwingine hajaruhusiwa kuishi au kufanya kitu kwenye eneo hilo

__  Kwa sababu wewe ndiye unayetaka kufanya jambo kwenye ardhi hiyo na ufanikiwe inakubidi uwe mhusika pia wa kufanya toba hiyo kumbuka

__  Lengo la toba hiyo ni ili mungu asamehe na kuomba adhabu ya ukiwa juu ya ardhi hiyo hali ya adhabu ya ukiwa ndiyo mara nyingi ( si mara zote lakini mara nyingi ) imefanya maeneo mengi ya ardhi yawe tupu na yasiendelezwe hata kama ni maeneo mengi ya ardhi yawe tupu na yasiendelezwe hata kama ni maeneo mazuri kwa kuishi au kwa kulima au kwa kufanyia biashara

Taarifa hiyo ya Roho Mtakatifu haikuzuii kununua au kutumia au kuliendeleza hilo eneo Bali, Roho Mtakatifu anataka ujue adhabu hiyo ipo kwenye ardhi na ni vinzuri ushughulikie hiyo adhabu, ili mungu aiondoe.

Ndiyo maana ukiliombea hilo eneo utaona moyoni mwako unasikia kuomba kwa kuomboleza ( yeremia 4:25 )

Hali hiyo ya kuomboleza ni ishara toka kwa Roho Mtakatifu ya kuwa ombea hilo eneo wala usipuuzie na maombi yako yakipata majibu toka kwa Mungu utasikia moyoni mwako huko kuomboleza kumeisha moyoni mwako na ukiwa hutausikia moyoni mwako utakapokuwa unaombea au umekanyaga eneo hilo la ardhi

Jambo hili ni muhimu kwa kuwa adhabu ya ukiwa ktk ardhi ya eneo infanya eneo hilo

__  Lisikaliwe na watu ( Ezekiel 33:28 ) ( yeremia 51:29 )

__  Lisitembelewe na watu ( zakaria 7:14 )

__  Kitu kitakachofanyika hapo kisizae matunda au matokeo yaliyokusudiwa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...