Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Roho mtakatifu part 3 Na Christopher Mwakasege

Jinsi Roho Mtakatifu Anavyotumia Moto Wa Mungu Ktk Kuongoza Mtu

Moto ndani yako kama ishara ya roho mtakatifu kukuhimiza usiache kufanya kile ambacho amekuingiza ukifanye, hata kama upinzani dhidi yako ni mkubwa ili usikifanye.
Nabii yeremia alikutana na hali ya namna hii, wakati wa kipindi alipokutana na upinzani dhidi ya utumishi aliokuwa amepewa na mungu upinzani huo ulimfikisha mahali pa kuona ya kwamba amekuwa kitu cha kuchekesha mchana kutwa ( yeremia 20:7 )
Nabii yeremia aliona kama vile neno la bwana limefanywa shutumu na dhihaka kwake mchana kutwa ( yeremia 20: 8 ) na kwa sababu hiyo anasema nami sitamtaja wala sitasema tena kwa jina lake ( yeremia 20: 9 ) kwa tafsiri nyingine upinzani dhidi ya utumishi aliopewa na mungu ulimfikisha mahali pa kuamua kutokusema tena kwa jina la mungu wala asimtaje mungu popote tena uamuzi huo haukumfanya mungu anyamaze bila kufanya jambo lililomwonyesha nabii yeremia ya kuwa mungu hakukubaliana n uamuzi wake ule.
Nabii yeremia anaeleza yaliyotokea hii nami nikisema sitamtaja wala sitasema tena kwa jina lake basi ndio moyoni mwangu kumekuwamo kama moto uwakao uliofungwa ndani ya mifupa yangu, nami siwezi kustahimili, wala siwezi kujizuia ( yeremia 20:9 )
Kwa tafsiri nyingine nabii yeremia alitaka tujue ya kuwa alipoamua kuacha kufanya alichotumwa na mungu kwa sababu ya upinzani dhidi yake.
Mungu aliwasha moto ndani yake ambao aliona kama vile umefungwa ndani ya mifupa yake na ujumbe wa mungu ktk moto ule ulikuwa ni wakumhimiza yeremia abadili msimamo wake wa kuacha kufanya kazi aliyopewa na mungu na badala yake aamue kuendelea kufanyabkazi kama alivyoelekezwa na mungu.
Hata katikati ya upinzani dhidi yake ukisoma vinzuri mstari huo, utaona ya kuwa yeremia hakukubali mapema kuufuata ujumbe wa mungu uliokuja kwake kwa njia ya ishara ya moto ndani yake ndio maana anasema juu ya moto ule ya kuwa nami siwezi kustahimili wala siwezi kustamili wala siwezi kujizuia.
Moto ule ulikuwa mkubwa sana moyoni mwake kiasi cha kuusikia ukiwaka na kufukuta kama vile umefungwa ndani ya mifupa yake.
Hali ile ya moto ule ilimfanya abadili uamuzi wake na akaamua aendelee kuifanya kazi aliyopewa aifanye na mungu.
Moto ule haukuja kumpa taarifa kuwa mungu atampa ushindi dhidi ya upinzani wake
Nabii yeremia anakiri kwa kinywa chake, juu ya ujumbe ulioingia moyoni mwake kwa njia ya moto wa mungu uliowaka ndani yake ya kuwa lakini bwana yu pamoja nami.
Mfano wa shujaa mwenye kutisha kwa hiyo hao wanaonionea watajikwaa, wala hawatashinda watatahayarika sana wataona aibu ya milele ambayo haitasauliwa kamwe ( yeremia 20:11 )
Kwa hiyo unapoacha au unaposikia kuendelea kuifanya kazi yabmungu uliyopewa kwa sababu ya upinzani dhidi yako unaokutana moyoni mwako moto huo moyoni mwako ni ishara ya roho mtakatifu ya kukupa ujumbe wa mungu kwako
____ Ya kuwa usiache kuifanya kazi ya mungu unayoifanya hata ikiwa umesongwa na upinzani mkubwa dhidi yako unaokukatisha tamaa usiendelee kuifanya

_____ Mungu yu pamoja nawe na atakupigania na kukupa ushindi dhidi ya upinzani uliokuandama
Ni maombi yangu kwa mungu kwamba anapokuwekea ishara ya moto wake moyoni mwako kwa njia Roho mtakatifu atakupa na ufafanuzi wake ili ujue moto huo una ujumbe gani wa kimaelekezo kwako kutoka kwake mungu.  Amina

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...