Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kilimo bora cha karoti

Asili ya zao hili ni persia ulaya na kusini magharibi mwa Asia kwa Tanzania zao hili hulimwa hasa mikoa ya Iringa, mbeya, morogoro, Arusha na kilimanjaro

HALI YA HEWA & UDONGO
Karoti zinahitaji hali isiyokuwa na joto sana, wala baridi sana, kati ya nyuzi za degree 15 mpaka 27 za sentigredi. Kama ukanda wa pwani unajoto kali, inatakiwa karoti zilimwe miezi ya majira ya baridi, karoti zinazotoka mazingira ya baridi huwa na radha nzuri pamoja na harufu nzuri. Udongo wa kichanga chepesi na tifutifu ndio unafaa ktk kilimo cha karoti, udongo wa mfinyanzi na udongo mzito hudumaza mazao

UTAYALISHAJI WA SHAMBA
Karoti zinahitaji shamba lilimwe kwa trekta, kwa ng'ombe ama kwa jembe la mkono kwa kina cha sentimita 30 hadi 45. Mkulima anatakiwa kuandaa matuta yenye mwinuko wa kimo cha sentimita 28, 40 kwenye shamba na upana wa mita 1 pia mita 15 umbali wa tuta moja hadi lingine. Kwa maandalizi mazuri tengeneza mifereji midogo ya kusiha mbegu za karoti yenye umbali wa sentimita 15 - 20, mifereji minne kwa tuta.

UTATALISHAJI WA MBEGU
Jinsi ya kujua mbegu nzuri zenye uwezo wa kukua bila wasi wasi. mbegu zenye uwezo wa kuota hutoa harufu kali unapozifikisha. Zilizopoteza uwezo wa kuota huwa hazitoi harufu yoyote ili mbegu ziote haraka ziloweke ktk maji kwa muda wa saa 24 baada ya hapo changanya Mbengu hizo na mchanga, Kwa kiasi kinacholingana ili kupata mtawanyiko mzuri wa mbegu wakati wa kupanda

UPANDAJI
Ina hitaji uoteshe kwenye kitalu ndipo uhamishie shambani weka Mbegu ktk chupa ya milimita 100 na toboa kidogo mfuniko, baada ya hapo changanya Mbegu ktk mifereji ya kupanda kwa kutumia mboji au mchanga, ukimaliza myunyiza maji ya kutosha, funika tuta na plastiki nyeusi, hatua nyingine kandamiza plastiki kwa pembeni na kwa mabonge ya udongo ili isipeperushwe na upepo. Mbegu huota baada ya siku 3 - 5 kutegemea na hali ya hewa. Inakupasa kukagua shamba mara tatu kwa siku. Baadaye ondoa plastiki mara moja pindi utakapoona mbegu moja tu iliyoota. Usicheliweshe kuondoa plastiki husababisha miche inayoota kufa kwa kuunguzwa na joto lililo ktk plastiki. Hapo tayari kwa kupanda shambani upandaji wa moja kwa moja shambani ktk matuta au sesa kiasi cha kilo 8 za mbegu kinatosha kupandwa kwenye Hekta moja.

MBOLEA
Weka mbolea aina za asili ( Samadi au mboji ) mwanzoni, ila kama haukutumia mbolea ya samadi au mboji weka mbole ya S/A kilogramu 100 kwa hekta kama haukutumia mbolea ya asili, kama ulitumia mbolea za asili basi weka kilogramu 50 kwa hekta kisha tumia NPK wiki sita baada ya kupanda. Matumizi ya mbolea za maji yafanyike kila baada ya wiki mbili kutegemea na mahitaji

UPANDAJI & UNYEVU
Ili kupata mavuno mengi palilia shamba mara kwa mara ili kuhakikisha shamba halina magugu na nyasi kwa kung'olea kwa mkono, jembe na mangineyo, na kwenye udongo hakikisha kuna unyevu wa kutosha kama sio kipindi cha mvua inatakiwa umwagilie shamba lako kwa wiki mara mbili

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...