Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Wapanda farasi wanne part 3

Juma lililopita tulijifunza mpanda farasi wa rangi ya moto.
Tukajua kazi zake na mamlaka yake yote amepewa na nani? Sasa leo tunaendele na mpanda farasi mwingine nayeni MPANDAJI WA FARASI MWEUSI.
Tutajua kazi yake ni nini ?  Ninakukaribisha rafiki yangu kuwa pamoja na mimi,  karibu sana.

MPANDAJI WA FARASI MWEUSI
" Nami nikaona,  na, tazama! Farasi mweusi, na yeye anayeketi juu yake alikuwa na mizani mkononi mwake. Nami nikasikia sauti kana kwamba ni katikati ya wale viumbe hai wanne ikisema: Kibaba cha ngano kwa dinari moja, na vibaba vitatu vya shayiri kwa dinari moja, na vibaba vitatu vya shayiri kwa dinari moja, wala usidhuru mafuta ya zeituni na divai." Ufunuo 6:5,6.
Mpanda farasi huyo anawakilisha njaa. Njaa imekithiri hivi kwamba kibaba cha ngano kinagharimu dinari moja, yaani, mshahara wa siku moja ktk karne ya kwanza! ( Mathayo 20:2 ) Dinari hiyo pia ingeweza kununua vibaba vitatu vya shayiri, nafaka ambayo haikuonwa bora kama ngano. Je kiasi hicho kingetosha familia kubwa? Kisha, watu wanaonywa kupima vyakula vya kila siku, vinavyowakilishwa na mafuta ya zeituni na divai ambavyo vilikuwa vyakula vya msingi nyakati hizo.
Tangu 1914 je, kuna mambo ya na horhi boyish a kwamba mpandaji wa farasi mweusi yuko mwendoni?  Ndiyo! Ktk karne ya 20, watu wapatao milioni 70 walikufa kutokana na njaa.
Shirika moja lilikadiria kuwa " watu milioni 805, yaani, mtu mmoja kati ya watu tisa duniani kote hakupata chakula chenye lishe kati ya mwaka wa 2012 - 2014. Ripoti nyingine inasema hivi: " Kila mwaka, njaa huua watu wengi zaidi kuliko jumla ya watu wanaokufa kutokana na UKIMWI, malaria na kifua kikuu." Iicha ya jitihada nyingi za kuwalisha wenye njaa, mpandaji wa farasi mweusi bado anaendelea na mwendo
Asante sana rafiki tukutane juma lijalo hapa hapa msikivu blog asante sana

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...