Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Chanzo cha Ganzi na kuchomwa na pini mwilini

Mojabya maswali ninayoulizwa na kulalmikiwa sana na watu wenye umri mkubwa ni uwepi wa ganzi na hisia za kuchoma na kama pini miguuni.

Ingawa dalili hizi zinaweza kutokea kokote pale mwilini ikiwemo mikononi, vidoleni, mabegani.
Kuna sababu nyingi za kujitokeza kwa hali hii ikiwamo pale unaposimama au kukaa mahali pamoja muda mrefu.
Majeraha ya shingo au pingiri za mgongo yanaweza kusababisha ganzi na kuchomachoma ktk mabega na mgongo.
Kama mtu atakuwa na majeraha ktk mgongo au kiuno anaweza pia kupata ganzi ktk maeneo ya miguuni.
Uwepo wa mgandamizo unaoleta shinikizo ktk mishipa ya fahamu inayotokea ktk uti wa mgongo mfano santuri za mgongo zinapi choropoka.
Shinikizo ktk mishipa ya fahamu baada ya kugandamizwa na mshipa ya damu uliotuna, uvimbe, kovu la tishu na uwepo wa uambukizi yote yanasababisha ganzi.
Maambukizo ya virusi vya mkanda wa jeshi, damu kuwa chache au kutofikia sehemu fulani mwili ikiwamo kujeruhiwa na theluji au mishipa ya damu kuharibika.
Kuwa na kiwango kisicho cha kawaida cha madini mbalimbali ikiwamo kalsiumu, potasiamu na sodiamu.
Ukosefu wa vitamini B na viatamini nyingine pamoja na virutubisho mbalimbali mwilini pia ni mojawapo ya ganzi mwilini .
Pia matumizi ya dawa za matibabu ikiwamo dawa za kifua kikuu ( TB ) na kufubaza makali ya VVU huambatana na hali hii.
Matibabu ya mionzi nayo yanambatana na kujitokeza kwa ganzi mwilini.
Vitu kama madini ya risasi, pombe na kemikali tiba za kutibu saratani huweza kusababisha ganzi mwilini kwani zina haribu mishipa ya fahamu.
Kuumwa na wadudu au wanyama ikiwamo nyoka, buibui, nge na aina ya mijusi wakubwa na jamii ya viumbe wa baharini pia kunaweza kuleta ganzi.
Maradhi ni kama vile kisukari, kipanda uso, ugonjwa wa kinga, kifafa nk
Asante sana juma lijalosuluhisho la ganzi hapa msikivu blog

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Utengenezaji wa sabuni

1: Utengenezaji wa sabuni za mche     Malighafi: 1: Caustic kg 4 2: Maji lita 10 3: Mafuta lita 20 4: Sodium Silicate Kg 2 5: pafyumu mili lita. 250 __  300 6: Chumvi vijiko 2 vikubwa Sabuni hii unaweza kuogea na kufulia inakuwa nzuri sana. Jinsi ya kutengeneza Loweka Caustic kg 4 kwenye maji ya lita 10 kwa siku 3. Ndani ya siku hizo tatu, utakuwa ukikoroga kila siku asubuhi na jioni kwa dakika 5. Kisha chukua sodium silicate kg2 ikifuatiwa na chumvi vijiko 2 vya chakula na mafuta huku unaendelea kukoroga kwa juhudi. Baada ya hapo weka kwenye maumbo kwa siku 3 __ 5 ili igande vizuri. Asante sana rafiki

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya unga

Sabuni ya unga Malighafi. A. Solphonic lita 1 B. Sodium sulphate kilo 3 C. Optical brightener vijiko 10 vya chakula D. Nausa vijiko 10 vya chakula E. Soda ash kilo 3 F. Pafyumu kijiko 1 cha chakula G. Rangi kijiko 1 cha chakula Jinsi ya kutengeneza Andaa malighafi kwa resho kama ilivyoandikwa hapo juu, Beseni na mwiko, kisha weka kimoja kimoja ukianza na herufi A __ G, huku ukikoroga mseto wako kwa muda wa dakika 15 halafu anika sehemu yenye hewa kivulini hadi ikauke. Hapo sabuni yako ya unga itakuwa tayari, iweke kwenye vifungashio ipeleke aokoni