Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ni faida kujisomea neno la mungu Na wilson mtishbi

Leo tutakumbushana jambo hili la kujisomea, kwa nini kujisomea?
Kujisomea ni ufahamu, kama huna ufahamu hutaweza kujisomea
Ktk kujisomea tunatoa ujinga tunaingiza mahalifa, Tuna jenga akili
( Mathayo 22:29 ) nasoma kwa jina la Bwana, " yesu akajibu akawaambia, mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa mungu "
Unapokosa kujisomea neno la mungu utakosa kujua uwezo wa mungu na nguvu zake, kila jambo kwako utakosa amani na imani na mungu wako.
Naweza kusema hivi kuwa vitendo vya kukata viungo vya walemavu wa ngozi sababu ya kujipatia utajili ni imani potofu,
Kwa maana hakuna mahali kwenye biblia palipo sema heti viungo vya walemavu wangozi vinzuri kwa kujipatia utajiri hakuna, hii ni imani potofu, sababu kubwa ni watu kutotaka kujisomea neno la mungu wanakosa ukweli wa mungu basi wanadanganyika na maneno ya shetani.
Leo ninakupa ufahamu ili uweze kujisomea kwa maana faida ipo Je unamfahamu Daniel ?
( Daniel 9:12 ) inasema hivi " Ktk mwaka wa kwanza wa Dario, mwana wa Ahasuero, wa uzao wamedi, aliyetawazwa kuwa mfalme juu ya milki ya wakaldayo ktk mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Daniel, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la BWANA lilimjia yeremia nabii, ya kutimiza ukiwa wa yerusalemu, yaani, miaka sabini. "
Kumbuka nilikuwambia hivi, huwezi kujisomea kama huna ufahamu, Daniel alikuwa na ufahamu ya kujisomea vitabu ndipo akafahamu hesabu inayo wapasa kuka utumwani, kwa maana wana israeli walikuwa utumwani kipindi.
Ipo faida ktk kujisomea MUNGU HAKUPE UFAHAMU ILI UWEZE KUJISOMEA
Penda kujifunza ili akili yako iwe na matunda ndugu
Asante sana rafiki

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Utengenezaji wa sabuni

1: Utengenezaji wa sabuni za mche     Malighafi: 1: Caustic kg 4 2: Maji lita 10 3: Mafuta lita 20 4: Sodium Silicate Kg 2 5: pafyumu mili lita. 250 __  300 6: Chumvi vijiko 2 vikubwa Sabuni hii unaweza kuogea na kufulia inakuwa nzuri sana. Jinsi ya kutengeneza Loweka Caustic kg 4 kwenye maji ya lita 10 kwa siku 3. Ndani ya siku hizo tatu, utakuwa ukikoroga kila siku asubuhi na jioni kwa dakika 5. Kisha chukua sodium silicate kg2 ikifuatiwa na chumvi vijiko 2 vya chakula na mafuta huku unaendelea kukoroga kwa juhudi. Baada ya hapo weka kwenye maumbo kwa siku 3 __ 5 ili igande vizuri. Asante sana rafiki

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya unga

Sabuni ya unga Malighafi. A. Solphonic lita 1 B. Sodium sulphate kilo 3 C. Optical brightener vijiko 10 vya chakula D. Nausa vijiko 10 vya chakula E. Soda ash kilo 3 F. Pafyumu kijiko 1 cha chakula G. Rangi kijiko 1 cha chakula Jinsi ya kutengeneza Andaa malighafi kwa resho kama ilivyoandikwa hapo juu, Beseni na mwiko, kisha weka kimoja kimoja ukianza na herufi A __ G, huku ukikoroga mseto wako kwa muda wa dakika 15 halafu anika sehemu yenye hewa kivulini hadi ikauke. Hapo sabuni yako ya unga itakuwa tayari, iweke kwenye vifungashio ipeleke aokoni