Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Usafi na ubora wa nguo

Nguo hutengenezwa kwa nyuzi zinazotoakana na utembo. Utembo huo hupatiakana kutoka kwa wanyama, mimea na mchanganyiko wa kemikali.

Utembo wa mimea hutupatia nguo za aina ya pamba na lineni. Utembo wa wanyama hutoa silki n sufu.
Utembo wa kemikali hutengenezwa nguo za utembo ni mashati, suruali, magauni, shuka, foronya, vyandarua, fulana na taulo.

Ufuaji nguo

Wakati wa kufua nguo ni muhimu kuwa waangalifu kwa sababu ya kuhifadhi muundo asilia wa nyuzi za nguo na vile vile rangi yake.
Hali kadhalika nguo hufuliwa kwa kuzingatia asili yake, iwapi ni nguo za pamba, sufu, silki, au nailoni.

Tendo la 1: kufua nguo nyeupe za pamba

Wakati wa kufua nguo za pamba lazima kuzingatia mambo muhimu kama vile tofauti ya nguo nyeupe za pamba au nguo za rangi.
Iwapo nguo ni nyeupe zifuliwe kama ifuatavyo.
Fua nguo hizo pekee bila ya kuzichanganya na nguo zo zote za rangi.

1. Loweka nguo kwa muda ili kulegeza uchafu.
2. Fua nguo hizo pekee bila ya kuzichanganya na nguo zo zote za rangi
3. Tumua sabuni yenye ditajenti kwa kuwa husaidia kung'ariaha nguo hizi
4. Chemsha kila inapolazimu, hasa zinapokuwa zimeanza kupoteza weupe wake
5. Suuza nguo vizuri na hakikisha sabuni imetoka vizuri
6. Tia bluu ktk nguo nyeupe kila inapolazimu
7. Anika nguo nyeupe za pamba juani baada ya kuzifua kwa sabuni, jua husaidia kuzitakasa, yaani kuzifanya nyeupe zaidi.

Tendo la 2: Kupiga pasi nguo nyeupe za pamba

Iwapo nguo zitapigwa pasi siku hiyo zianue kabla hazijakauka kbisa.
Zikunje kwa marefu yake kisha ziviringishe sana. Iwapi utazipiga pasi ktk siku inayofuata ziache juani kwenye kamba mpaka zikauke kabisa ndipi uzianue.

1. Nyunyuzia maji ktk nguo zilizokauka kabisa kisha ziviringishe ili unyevu uenee ktk nguo.

2. Tayarisha vifaa vyote vinavyotakiwa kwa kupuga pasi.

3. Anza kupiga pasi kwa ndani ktk sehemu zilizo maradufu kama vile, pindoni, kwenye sijafu na kwenye majongo. Sijafu ni pindo la ndani la mkono wa kanzu au koti.

4. Geuza nguo na piga pasi nguo yote ktk upande wa nje kwa kufuata nyuzi za matande.

5. Tandaza za nguo ziweze kupata hewa na kukauka sawasawa.

6. Kunja na weka sandukuni au kabatini.

Tendo la 3: Kufua nguo za nailoni

Nguo za namna hii mara nyingi ni imara na nyepesi. Haziruku wala haziharibiki umbo lake wakati wa kufuliwa.

Huweza kuyeyuka zikipata moto na kuweka makunyanzi ya kudumu zikipata joto kali.

1. Fua nguo ktk maji moto yenye povu la sabuni au ditajenti.
2. Fua kwa kufikicha nguo katikati ya mikono bila kusugua.
3. Suuza nguo ktk maji vuguvugu hadi povu litoke. Mwisho suuza ktk maji baridi.
4. Anika nguo bila kukamua iwapi ni za rangi anuwai. Zianike kivulini.
5. Nguo za nailoni hazipigwi pasi. Ikibidi kuzinyoosha tumia pasi yenye joto kidogo.

Asante sana

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Utengenezaji wa sabuni

1: Utengenezaji wa sabuni za mche     Malighafi: 1: Caustic kg 4 2: Maji lita 10 3: Mafuta lita 20 4: Sodium Silicate Kg 2 5: pafyumu mili lita. 250 __  300 6: Chumvi vijiko 2 vikubwa Sabuni hii unaweza kuogea na kufulia inakuwa nzuri sana. Jinsi ya kutengeneza Loweka Caustic kg 4 kwenye maji ya lita 10 kwa siku 3. Ndani ya siku hizo tatu, utakuwa ukikoroga kila siku asubuhi na jioni kwa dakika 5. Kisha chukua sodium silicate kg2 ikifuatiwa na chumvi vijiko 2 vya chakula na mafuta huku unaendelea kukoroga kwa juhudi. Baada ya hapo weka kwenye maumbo kwa siku 3 __ 5 ili igande vizuri. Asante sana rafiki

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya unga

Sabuni ya unga Malighafi. A. Solphonic lita 1 B. Sodium sulphate kilo 3 C. Optical brightener vijiko 10 vya chakula D. Nausa vijiko 10 vya chakula E. Soda ash kilo 3 F. Pafyumu kijiko 1 cha chakula G. Rangi kijiko 1 cha chakula Jinsi ya kutengeneza Andaa malighafi kwa resho kama ilivyoandikwa hapo juu, Beseni na mwiko, kisha weka kimoja kimoja ukianza na herufi A __ G, huku ukikoroga mseto wako kwa muda wa dakika 15 halafu anika sehemu yenye hewa kivulini hadi ikauke. Hapo sabuni yako ya unga itakuwa tayari, iweke kwenye vifungashio ipeleke aokoni