Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Pango la kike la mfupa wa nyonga ( The female pelvis )

Tujifunze kwa bidii ktk picha na ktk mifupa sura yake sehemu zake na eneo lake.
Tukiisha ya jua hayo tutavifahamu vizuio vingi vipatikanavyo wakati wa uzazi, kwa kuwa mtoto hulazimishwa kuputia ktk sehemu moja wapo nyembamba ya pango anapozaliwa.

Sura ya mifupa ya pango la nyonga

1.  Mfupa wa pingili za nyonga upande wa nyuma ( the sacrum )

2.  Mfupa wa kifandugu upande wa chini ( the coccyx )

3.  Mifupa miwili ya nyonga kwa kila upandea ( the innominatebones )

1.  Mfupa wa pingili za nyonga ni maendeleo ya uti wa mgongo zakaa ktk mfereji wake na zatoka ktk vitundu vyake. Mfupa huu umebonyea na watunga ukuta wa nyuma wa pango la nyonga kwa juu unagusana na pingili ya tano ya kiuno. Ukingo wake umechongoka kama nundu na unajibenua kwa ndani ya pango.
Nundu na unajibenu kwa ndani ya pango. Nundu hiyo yaitwa rasi ya nyonga.
Rasi hiyo ina maana sana wakati wa kuzaa, kwa sababu ikijitanua zaidi kwa ndani, eneo la mlango wa pango linapungua. Hivyo kichwa cha mtoto hupita kwa shida na pengine huzuiwa kabisa

2.  Mfupa wa kifandugu ni maendeleo ya pingili za nyonga na mkia wa uti wa mgongo. Sehemu zake ni pingili 4-5 ndogo sana na zasaidia kufanya msingi wa pango.
Zanyoosheka zinapogusana na mfupa wapingili za nyonga.
Hivyo kichwa cha mtoto kinapopita hapa kinasukuma kifandugu kwa nyuma na pango hutanuka kiasi cha cm 1 hata 1.5

3.  Mifupa miwili ya nyonga ni mikubwa,upo mmoja kila upande na yaungana kwa mbele. Ktk utoto kila mmoja una sehemu tatu zinazoungana ktk utu uzima, yaani wakati wa umri wa miaka 20.

Kila sehemu ina jina lake ndilo:

1.  Kombe la kiuno ( the ilium )
2.  Mfupa wa kinena ( the pubic bone )
3.  Mfupa wa kukalia ( the ischium )

a.  Makombe mawili ya kiuno ni mifupa mikubwa ya bapa na yafanana na bakuli kubwa pasipo msingi. Ukingo wake wa nje wapapasika chini ya mbavu kiunoni ( the iliac crest ) na waishilia kwa mbele na kwa nyuma kwa nundu.

Nundu za mbele za kiuno ( the anterior superior spines ) za papasika penye tumbo kwa juu ya kinena.
Nundu za nyuma za kiuno ( the posterior superior spines ) zapapasika mgongoni karibu ya pingili ya 4 ya kiuno. Kwa mbele makombe yaenea ktk mifupa y kinena.
Kwa ndani makombe yana ukingo uliovirigana ( the pelvic brim ) ukingo huu pamoja na mifupa ya kinena na mfupa wa pingili za nyonga watunga mlango wa pango la kweli.

b.  Mifupa ya kinena ni midigo, myembamba na ya bapa. Hiyo ni ya panda nayo yaacha tundu ya kinena ndiyo itungayo sehemu ya mbele ya pango nayo imeunganishwa kwa kano shupavu ya mfupa ( symphysis ) ukingo wa chini ya mifupa hiyo umekunjika mfano wa uta ( the pubic arch )

c.  Mifupa miwili ya kukalia ni minene tena butu nayo yafanya sehemu ya chini na ya nyuma ya pango.
Tukaapo twaitegemea. Kila mfupa wa kukalia una nundu nyembamba zielekeazo mbele kidogo nazo zapapasika kama miiba tuingizapo vidole ukeni ( the ischiatic spines )

Tulivyoona sehemu ya nyonga imekazwa katikati kwa ukingo kadiri ya kutunga mapango mawili.
Pango la juu lafanana na bakuli pana ndimo matumbo yakaamo, pia wakati wa uja uzito mimba yakaa humo. Ktk lile pango la chini ndimo vikaamo viungo vya uzazi, kibofu na mwisho wa utumbo mpana

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...