Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mkunga ( the Midwife )

Wanawake, watu wazima na vijana, watakao kazi ya ukunga wafahamu kuwa kazi yao yaheshimiwa sana wakiwa hodari na waaminifu.
Lakini wale walio dhaifu, wavivu, wenye akili ndogo au wafadhaikao upesi na kudharau. Sheria ya mungu, hawa hawafai hata kidogo.

Mkunga yampasa awe au ajibidishe kuwa na hali pamoja na tabia hizi

1.  Awe na afya njema na hodari: Inamlazimu kukesha mara nyingi bila kulala.
Pengine ataitwa kwenda safari kwa miguu kusaidia wazazi mjini.

2. Awe na apende usafi na utaratibu: Kwake yeye mwenyewe na vitu atunzavyo. Avae nguo safi toka juu mpaka chini. Anawe hasa mikono na kusafisha kucha na kuzikata mara kwa mara .
Akiwamo katika chumba cha kupasulia ( operating Theatre ) Amwuguzapo mzazi aliyekwisha kuzaa akumbuke mafundisho kuwa. Baada ya kuzaa hubakia kidonda kikubwa ktk mji wa mimba, basi aangalie asiinhize vijidudu humo.

3.  Awe mwenye akili na bidii:
Yaani apate kufahamikiwa na mafundisho na ajue kuyatumia, afahamu kuwa kusoma hakuna mwisho, aendelee kutaalamika kila anapoanfalia mara nyingi kwa akili kila namna ya uzazi, na ndipo apatapo ustadi.
Ni wajibu kwa mkunga kuangalia maendeleo ya uzazi, kumpima na kuandika habari za mzazi; aziandike na kuzisema habari halisi zisiwe za uwongo ay za ovyo ovyo. Inambidi vile vile kufahamu na kutambua upesi hatari za maisha ya mtoto na mama pia

4. Awe na moyo, mwenye huruma na upole: angalie mahitaji yote ya mzazi, kiu, jasho, haja, na kuchoka kwake.
Pasipo kuombwa, ampekinywaji; amkaushe jasho na kumnawisha au kumwogesha, ampe chombo cha haja kila ahitajipo. Mara kwa mara amtengenee mito na tandiko la kitanda, akimtegemeza vizuri mgonjwa. Asiwe mkali wala mwenye kukasirika pasipo sababu, akumbuke kuwa akiwa mpole atamtuliza mazazi, kila mara akumbuke mahangaiko na maumivu ya mzazi.

5.  Awe shujaa: kwa kuwa atapata kuona mambo ya hatari yanayotisha ya maisha ya mtoto au mama mzazi. Kufadhaika, kulia na kukimbia hakuna faida. Lazima awe shujaa asaidie kwa kila namna na labda asingaliwapa msaada wangalikufa.

6.  Amche Mungu na sheria zake: Twafahamu mimba ni kweli mtoto wa kibinadamu toka kuungana mbegu na kijiyai. Tena mimba si sehemu au kiungo cha mama kama mkono au tumbo. Aidha mfumo yawezekana ya kuwa damu ya mtoto haipatani na damu ya mama, bali na baba na kadhalika kwa ufupi mimba ni kiumbe kilicho mbali mbali na mama kuua mimba ni kumwua mtoto mchanga aliyekwisha zaliwa. Mkunga aheshimu maisha hayo ya mimba na kwa vyovyote vile asitoe msaada wa kuiharibu mimba, yaani kuitoa.
Mkunga aonapo kuhangaika na machungu mengi ya wazazi na pia furaha na upendo mwingi kwa watoto wao akumbuke baraka za ndoa; kuwa ktk ndoa wazazi hupata nguvu za kuwa na upendo huo na ikiwa yeye mwenyewe hajaolewa bado asijiachilie kuwa mkunga ataata baraka ya kazi zake akiwa mwenyewe anamcha mungu na sheria zake.

Asante sana kwa leo tunaishia hapa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...