Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mbinu za kupata mtaji wa biashara

Watu wengi wanatamani kumiliki biashara siku moja na huenda wana mipango minzuri juu ya biashara zoa mipango hii inaweza ikwa vichwani tu au mingine ktk maandishi.
Lakini inapofikia wakati wa utekelezaji wa mipango hii ukosefu wa mtaji wa biashara hiyo ni kipingamizi kwa wengine
Lakini kuna jinsi kadhaa ambazo zinaweza kusaidia upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya biashara

Aina za mitaji

Kuna aina mbili ya mitaji kwa ajili y biashara au uwekezaji wa aina yoyote

__  Myaji wa mkopo
__  Mtaji wa mmiliki

Mtaji wa mkopo unakuwezesha kukopa toka kwa taasisi za fedha au mtu binafsi wa kiwemo ndugu jamaa na marafiki na kuhitajika kulipa ktk kipindi maalumu ikiwa pamoja na riba au bila riba

Aina hii ya mtaji inakuwezesha kufanya biashara lakini ni lazima uwe makini ktk utunzaji wa fedha zako na uzalishaji wake kwani mwishowe utahitajika kurudisha fedha zote pamoja na riba pengine kila mwezi.

Mtaji wa mmiliki ni mtaji toka kwa mtu au kampuni ambayo inahitaji kuwa na umiliki wa sehemu ya biashara. Hawa wanataka kupata faida kutokana na uwekezaji ktk kampuni au biashara yako.

Kama uko tayari kutoa sehemu ya umiliki wa biashara yako basi mtaji wa aina hii utakusaidia kuanzisha au kuboresha biashara yako.

Changamoto za kupata mitaji

Kupata mtaji wa biashara ni changamoto kubwa kwa wa jasiriamali kote duniani.
Japo fedha za mikopo zinapatikana ktk mabenki lakini biashara nyingi hazina miundo minzuri na mifumo ya fedha kuwezesha kupata mikopo.
Benki zimekuwa na masharti magumu sana kiasi kwamba biashara nyingi haziangalii huko kama sehemu ya kupata mikopo

Mikopo toka kwa ndugu na jamaa pia ina changamoto zake, si rahisi ndugu au rafiki akakuamini au akaamini kuwa biashara yako itafanikiwa, tunajua asilimia 90 za biashara zinazoanza zinakufa kila mwaka.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Utengenezaji wa sabuni

1: Utengenezaji wa sabuni za mche     Malighafi: 1: Caustic kg 4 2: Maji lita 10 3: Mafuta lita 20 4: Sodium Silicate Kg 2 5: pafyumu mili lita. 250 __  300 6: Chumvi vijiko 2 vikubwa Sabuni hii unaweza kuogea na kufulia inakuwa nzuri sana. Jinsi ya kutengeneza Loweka Caustic kg 4 kwenye maji ya lita 10 kwa siku 3. Ndani ya siku hizo tatu, utakuwa ukikoroga kila siku asubuhi na jioni kwa dakika 5. Kisha chukua sodium silicate kg2 ikifuatiwa na chumvi vijiko 2 vya chakula na mafuta huku unaendelea kukoroga kwa juhudi. Baada ya hapo weka kwenye maumbo kwa siku 3 __ 5 ili igande vizuri. Asante sana rafiki

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana