Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Maoni ya Biblia kuhusu Uhai na kifo Na Wilson Mtishbi

Simulizi la uumbaji kwenye kitabu cha mwanzo ktk Biblia linasema kwamba adamu, mwanadamu wa kwanza, aliambiwa hivi na mungu: " matunda ya kila mti wa bustani unaweza kula mpka ushibe.
Lakini kuhusu matunda ya mti wa ujunzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula, utakufa hakika" ( mwanzo 2:16,17 )
Maneno hayo yanaonyesha waziwazi kwamba iwapo Adamu angetii amri ya mungu, hangekufa bali angeendelea kuishi ktk bustani ya Edeni.
Kwa kusikitisha, badala ya kuchagua kutii ili aishi milele, Adamu aliamua kupuuza amri ya mungu na kula tunda alilokatazwa baada ya kupewa tunda hilo na hawa, mke wake. ( mwanzo 3:1,6 )
Madhara ya kutotii amri hiyo yanatuathiri sisi pia.

Mtume paulo alielezea hali hiyo hivi: " kupitia mtu mmoja dhambi iliingia ktk ulimwengu na kifo kupitia dhambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya dhambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya dhambi ( warumi 5:12 )
Bila shaka, " mtu [ Huyo ] mmoja ni Adamu.
Hata hivyo, alifanya dhambi gani, na kwa nini ilileta kifo?

Jambo ambalo Adamu alifanya. Yaani, kukataa kimakusudi kumtii mungu au kuvunja sheria yake, ni dhambi. ( 1 yohana 3:4 ) Na kama ambavyo mungu alikuwa amemwambia Adamu, adhabu ya dhambi ni kifo.
Ikiwa adamu na wazao ambao angepata baadaye wangeendelea kutii amri ya mungu,hawangekuwa na dhambi na kwa hiyo hawangepatwa na kifo.
Mungu hakuwaumba wanadamu wafe, bali waishi milele.

Kama Biblia ilivyosema hakuna shaka kwamba kifo " [ Kimeenea ] Kwa watu wote " lakini je, kuna sehemu fulani ya mwanadamu unayoendelea kuishi baada ya mtu kufa?
Huenda wengi wakajibu ndiyo, kwamba sehemu fulani inayoitwa nafsi, haifi.
Lakini hilo lingemaanisha kwamba mungu alimdanganya adamu. Jinsi gani?
Ikiwa sehemu fulani ya mwanadamu huendelea kuishi mahali pengine baada ya kifo, basi haingekuwa kweli kwamba kifo ni adhabu ya dhambi, kama mungu alivyomwambia adamu.
Biblia inasema: " mungu hawezi kamwe kusema uwongo." ( waebrania 6:18) Ukweli ni kwamba shetani ndiye aliyesema uwongo alipomwambia Hawa hivi: " Hakika hamtakufa." ( mwanzo 3:4 ) Hivyo basi swali ni; ni nini hutendeka mtu anapokufa?

Asante sana kwa uwepo wako.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Utengenezaji wa sabuni

1: Utengenezaji wa sabuni za mche     Malighafi: 1: Caustic kg 4 2: Maji lita 10 3: Mafuta lita 20 4: Sodium Silicate Kg 2 5: pafyumu mili lita. 250 __  300 6: Chumvi vijiko 2 vikubwa Sabuni hii unaweza kuogea na kufulia inakuwa nzuri sana. Jinsi ya kutengeneza Loweka Caustic kg 4 kwenye maji ya lita 10 kwa siku 3. Ndani ya siku hizo tatu, utakuwa ukikoroga kila siku asubuhi na jioni kwa dakika 5. Kisha chukua sodium silicate kg2 ikifuatiwa na chumvi vijiko 2 vya chakula na mafuta huku unaendelea kukoroga kwa juhudi. Baada ya hapo weka kwenye maumbo kwa siku 3 __ 5 ili igande vizuri. Asante sana rafiki

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya unga

Sabuni ya unga Malighafi. A. Solphonic lita 1 B. Sodium sulphate kilo 3 C. Optical brightener vijiko 10 vya chakula D. Nausa vijiko 10 vya chakula E. Soda ash kilo 3 F. Pafyumu kijiko 1 cha chakula G. Rangi kijiko 1 cha chakula Jinsi ya kutengeneza Andaa malighafi kwa resho kama ilivyoandikwa hapo juu, Beseni na mwiko, kisha weka kimoja kimoja ukianza na herufi A __ G, huku ukikoroga mseto wako kwa muda wa dakika 15 halafu anika sehemu yenye hewa kivulini hadi ikauke. Hapo sabuni yako ya unga itakuwa tayari, iweke kwenye vifungashio ipeleke aokoni