Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mambo yanayokuzuia kupata furaha ya kweli maishani mwako

Inaweza kuonekana ni kitu cha kawaida lakini kuwa na furaha ya kweli na ya kudumu ni kitu ambacho kinatafutwa sana na watu wengi.
Ndio maana ukichunguza, harakati nyingi za kutafuta maisha zinalenga hasa kupata furaha, hata hivyo pamoja na watu wengi kuitafuta furaha sana, lakini bado wengi pia wanaendelea kugubikwa na huzuni ni kiwa na maana ni watu ambao wanaishi maisha hayana furaha sana kwa sehemu kubwa Je, hebu tujiulize ni mambo gani ambayo yanasababisha mtu mmoja akawa na furaha au mwingine akaikosa furaha majibu ya maswali haya utayapata kwenye makala haya. Kikubwa fuatana nami tuweze kujifunza pamoja.

1.  Kufanya kazi usiyoipenda

Ipo asilimia kubwa sana ya watu ambao wanafanya kazi ambazo mara nyingi wanakuwa hawazipendi sana kwa lugha halisi wanakuwa ni watu wanafanya kazi ambazo hawazifurahii kikubwa kwao inakuwa ni kutaka kuingiza kipato tu, basi kama unafanya kazi ya namna hii ambayo huifurahii Lakini lengo lako ni kuingiza kipata basi elewa unabeba moja ya kitu ambacho kinakuzuia kupata furaha ktk maisha yako kwa namna moja au nyingine.
Watu wote wenye mafanikio wanafanya vile vitu ambavyo wanavipenda kutoka moyoni mwao, kama hufanyi kitu unachokipenda uwe na uhakika utaanza kujenga furaha yako

2.  Kujilinganisha na wengine

Ni tabia ya wengi wetu tangu tukiwa watoto wadogo kutaka kujilinganisha na watu wengine. Kwa bahati mbaya tabia hii imekua ikikua hadi kuweza kufikia ukubwani na wengi wetu tena tumekuwa tukiindeleza pasipo hata kujua. Mara nyingi tumekuwa tukijilinganisha ktk vipato vyetu tumekuwa tukijilinganisha ktk mavazi na mambo mengine, uchungu nzima hivyo, hutokana na kujiinganisha huko sana imekuwa ikipelekea sisi kukosa furaha kikawaida huwezi kuwa na furaha kama kila wakati unajilinganisha na wengine.
Maisha na furaha yako inabaki kuwa yako kama kweli unaishi wewe kama wewe kujilinganisha na wengine ni sawa na kutengeneza mazingira ya kupoteza furaha yako moja kwa moja

3.  Kuogopa mambo mengi

Ni asili ya binadamu kuwa na hali fulani ya woga kuna wakati tunakuwa tunakuwa tunogopa kujiingiza ktk jambo fulani, mathalani hata uthubutu wa kufanya kitu fulani, sasa inapotokea unakuwa ni mtu wa kuogopa sana mambo mengi na kila wakati, hiyo inakuwa ni changamoto moja wapo ambayo inakuzuia moja kwa moja wewe kuweza kupata furaha ya kweli, furaha ya kweli mara nyingi inapatikana hasa kwa wewe unapokuwa huru na mambo yako.
Unapokuwa huru huna hofu ya mambo mengi na kuishi kwa kujiamini hapo ndipo unakuwa na furaha ya kweli.

4. Kuishi wakati ulipita

Kuna watu ambao wengi wetu badala ya kuishi sasa, hujikuta ni watu wa kuishi kwa kukumbusha sana matukio mengi yaliyopita kama unaishi hivi kwa kukumbuka mambo mengi yaliyopita na ambayo yalikuumiza kwa namna moja au nyingine uwe na uhakika furaha yako utaipoteza.
Kujenga furaha ya kweli unatakiwa kuishi sasa na wala si kesho.
Fanya mambo yako kwa kuzingatia sana sasa watu wengi wenye mafanikio na furaha ya kweli wanaishi sasa na kusahau mambo mengine yaliyopita kumbuka wewe ndiye unayewajibika na kutengeneza furaha ya kweli wanaishi sasa na kusahau mambo mengi yaliyopita kumbuka wewe ndiye unaye wajibika na kutengeneza furaha ya kweli ktk maisha yako. Zingatia mambo hayo yanayokuzuia kupata furaha ya kweli

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...