Ktk karne ya kwanza, mtume paulo alitoa onyo hili: " Neno lililoongozwa na roho linasema kwa hakika kwamba ktk vipindi vya nyakati za mwisho wengine wataanguka kutoka kwenye imani, wakisikiliza maneno yaliyooongozwa kwa roho yenye kupitosha na mafundisho ya roho waovu" ( 1Timotheo 4:1 ) Bila shaka, maneno hayo yalithibitika kuwa ya kweli!
Fundisho la kutokufa kwa nafsi ni moja kati ya " mafundisho ya roho waovu." Biblia haiungi mkono fundisho hilo, na chanzo chake ni falsafa na dini za kale za kipagani.
Kwa kupendeza, Yesu alisema hivi kutuhusu:
" Nanyi mtaijua kweli, nayo kweli itawaweka ninyi huru." ( Yohana 8:32 ) Tunapopata ujuzi sahihi wa kweli ya Biblia, tunawekwa huru kutokana na mafundisho yasiyomheshimu mungu na mazoea ya nayoungwa mkono na dini nyingi za ulimwengu huu.
Kwa kuongezea, kweli iliyo ktk Neno la mungu inatuweka huru kutokana na utumwa wa tamaduni na ushirikina unaohusianishwa na kifo.
Muumba wetu hakukusudia wanadamu waishi duniani kwa miaka 70 au 80 na kisha waende kuishi milele mahali pengine.
Kusudi kuu la mungu ni kwamba wanadamu waishi milele hapa duniani wakiwa watoto wake watiifu.
Kusudi hilo linaonyesha jinsi ambavyo mungu anawependa wanadamu na hakika lutatimua. ( malaki 3:6 )
Mtunga zaburi aliongozwa kutangaza maneno haya yenye kutia moyo:
" waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake" __ Zaburi 37:29
Asante sana
Maoni
Chapisha Maoni