Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Haya ndiyo mambo muhimu anayopaswa kuyazingatia bibi harusi

Harusi ni sherehe ndefu, kuna mambo mengi ambayo hufanyika ktk kipindi hiki muhimu hususani kwa wanandia.
Kila mmoja huwa ana majukumu yake ktk kuhakikisha sherehe inafabyika kwa ukamilifu.
Haya hapa ni baadhi ya majukumu ya msingi kwa bibu harusi.

Tumia vizuri wapambe wako

Waombe wakufuatilie kwa karibu hasa kwenye sherehe ili usitumie muda nwingi kuzungumza na wageni au mgeni mmoja, lakini kujua mahitaji yako siku hiyo muhimu.

Piga picha kabla ya kuanza kwa sherehe

Zipo faida kadhaa za kufanya jambo hili kwanza kabla ya kuendelea kwa sherehe.
Kubwa zaidi ni kupata mapambo halisi ya bibi harusi kabla hajachoshwa na muzunguko.
Hata kama picha nyingine zitafutia. Lakini hizi za mwanzo huwa na mvuto zaidi.

Kuwa huru na mavazi yako

Hakikisha unavaa kile kinachokuweka huru. Vaa viatu vinavyokutosha, vaa gauni linalokukaa vizuri.
Hii itakufanya uwe na raha muda wote, kwani ule wasiwasi wa kudhani hauko sawa utakuwa haupo.
Mara nyingi haya huchangia kumfanya bi harusi asiwe na utulivu.

Usisahau kula

Hakikisha unakula chakula cha asubuhi cha kutosha. Pia si vibaya kubeba vitafunwa vya kiba endapo utasikia njaa

Weka mbali simu yako

Wakati mwingine simu inaweza kukuchanganya. Ni vyema ukaiweka mbali ili kujikita zaidi na mambo ya harusi

Hakikisha unakuwa wa kwanza

Kumbuka hii ni siku yako. Hivyo hakikisha furaha yako inakuwa jambo muhimu sana.
Unatakiwa kujitanguliza kwa kila kitu. Ni siku yako na haitakuja mara ya pili

Fahamu mazingira ya eneo uliopo

Pamoja na kuwa na wasaidizi, ni vyema ukaelewa eneo ulilopo na kuongeza umakini.
Kwa mfano unapotembea ni vizuri kufahamu eneo lina ngazi ama kuteleza

Furahia

Ni siku yako, na watu wote walioko mbele yako wamekufuata wewe. Onyesha furaha.
Asante sana

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Utengenezaji wa sabuni

1: Utengenezaji wa sabuni za mche     Malighafi: 1: Caustic kg 4 2: Maji lita 10 3: Mafuta lita 20 4: Sodium Silicate Kg 2 5: pafyumu mili lita. 250 __  300 6: Chumvi vijiko 2 vikubwa Sabuni hii unaweza kuogea na kufulia inakuwa nzuri sana. Jinsi ya kutengeneza Loweka Caustic kg 4 kwenye maji ya lita 10 kwa siku 3. Ndani ya siku hizo tatu, utakuwa ukikoroga kila siku asubuhi na jioni kwa dakika 5. Kisha chukua sodium silicate kg2 ikifuatiwa na chumvi vijiko 2 vya chakula na mafuta huku unaendelea kukoroga kwa juhudi. Baada ya hapo weka kwenye maumbo kwa siku 3 __ 5 ili igande vizuri. Asante sana rafiki

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana