Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Fanya yafuatayo kama umekuwa na siku mbaya

Tunaamini kabisa kwamba siyo siku zote huwa zinafanana mara nyingine siku huanza vema na kuendelea kwa furaha amani na mafanikio hadi mwisho wa siku hiyo mara nyingine siku yako huanza vibaya na kuishia vizuri.
Lakini ziko siku ambazo huonekana kuanza kwa mabalaa kama vile bahati mbaya, kupoteza vitu kuumia au huzuni ya moyoni na wengine hutabiri muonekano wa siku nzima kuanzia kwa yale yaliyojiri asubuhi.
Waswahili wamesema siku njema, huonekana asubuhi maana yake, mara nyingine hata siku mbaya pia hujionyesha ktk mawanzo wa siku hiyo.
Najua kuna baadhi ya imani zisizo rasmi ambazo hujaribu kulielezea suala hii mfano, ukiona bundi asubuhi au ukipishana na nyoka njiani.
Basi kuna walakini na siku yako hiyo.
Wapo wengine hasa wazungu ambao husema " ameamkia upande mbaya wa kitanda " sina uhakika kama kuna upande mbaya na mzuri wa kitanda.
Nia yangu ni kujaribu kukupa namna za kitaa laamu zinazoweza kukusaidia kuigeuza siku yako iliyoonekana kuanza vibaya kuwa nzuri na kupunguza pia uwezekano wa kuwepo kwa hizi siku zinazoaminiwa kuwa mbaya mswali

__  Je umewahi kukatishwa tamaa na kitu chochote mwanzoni mwa siku

__  Je umewahi kupoteza kitu mwanzoni mwa siku

__  Je umewahi kuumia moyo kwa kupata matarajio hewa ( disappointment ) mwazoni mwa siku au ktk siku fulani

__  Je umeshawahi kufanya kitu fulani na baadaye ukajutia kukifanya kitu na ukajihisi kushindwa au kuaibika

__  Umeshawahi kudhamiria kuingia kwenye uhusiano kwa matumaini yote na mara ukaona kila kitu kuwa ndivyo sivyo au umeshapitia matatizo fulani ya mwili, kama vile ugonjwa, ukilema ukaona labda ndiyo chanzo cha ugumu wa maisha yako.

Kama wewe ni mmoja wa watu hao basi karibu ktk ulimwengu wa wanadamu wa kawaida.
Wakati tunaposhindwa au kujihisi tumeshindwa mara nyingi tunadhani sisi peke yetu ndiyo tu wenye hali hiyo, ukweli ni kwamba, wengi hupitia huko na yamkini ktk hali ngumu zaidi
Kila fulani kila mmoja wetu amewahi kujutia jambo fulani alilolifanya kila mmoja wetu amewahi kukutana na magumu

Mambo ya kuzingatia

Jikubali kama mwanadamu wa kawaida na kwamba haistajabishi kushindwa yamkini unakata tamaa maana umezungumza na watu wanaoshinda na kufanikiwa tu
Angalia upande wa pili zungumza pia na waliowahi kushindwa .
Haijalishi ni muda gani ni kiasi gani ni ukubwa gani ni uzito kiasi gani wa magumu uliyopitia. Ninachojua ni kwamba inawezekana mimi na wewe kunyanyuka tena toka kushindwa kwetu, ndoto zetu zaweza kuwa kweli tena hii inategemea na kiasi uvumilivu wako
Tatizo siyo kushindwa kwa ukweli ni kule kushindwa kunyanyuka tena mara baada ya kushindwa mara ya kwanza Angalia mchezo wa ngumi, haijalishi mtu anapigwa na kuanguka mara nyingi kiasi gani, lakini pale anaposhindwa kunyanyuka ndiyo refa hutangazwa KNOCK OUT yaani ameahinda kabisa

Ili kuweza kunyanyuka tena

Jikubali kama mwnadamu wa kawaida tambua kushindwa kupo na ni moja ya matukio ya maisha yetu
Unapoanguka chini, jitahidi usibaki chini ( tofautisha kuanguka kwa mtoto na mtu mzima ) fahamu kushindwa kwa kweli ni kule kushindwa kunyanyuka mara baada ya kuanguka .
Jifunze, pata shule kupitia mapito na magumu unayoyapitia tatizo pia siyo kufeli, bali ni kufeli kujifunza ktk kule kufeli. Kufanya kushindwa kwako kuwe kama mawe ya kukanyagia ktk kuvukia kwenda upande wa pili.

"Tutakushangaa, ukiangushwa na jambo lile lile linalokuangusha mara zote"

Jifunze kutumainia ktk imani uliyonayo imani ni injini isiyoshindwa ktk suala zima la kushindwa na kuweza.
Imani huwa poozeo kwa maumivu tunayoyapitia

__  Jitahidi, vuta zaidi kazana amini kuwa kitu chema cha weza kutoka ktk mikono yako midomo yako, moyo wako au hata mawazo yako.

Asante sana kw leo tunaishia hapa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...