Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Somo Roho mtakatifu part 4 Na christopher Mwakasege

Jinsi Roho Mtakatifu Anavyomuongoza Mtu, kwa Kutumia Moto Wa Mungu

Moto wa mungu unapowaka ndani ya moyo wa mtu ukiwa umebeba taarifa ya ghadhabu na maonyo ya mungu.
Tunasoma katika ( Isaya 66:15 ) Ya kuwa maana Bwana atakuja na moto ili atoe malipo ya ghadhabu yake kwa moto uwakao na maonyo yake kwa miali ya moto.
Bwana atakuja na moto ina maana ya mungu kujifunua kwa njia ya au kwa ishara ya moto na ktk kujifunua huko ndani ya moto huo kuna ujumbe au taarifa ya malipo ya ghadhabu yake na maonyo yake kwa tafsiri iliyo rahisi utaona ya kwamba moto wa jinsi hii.
Unapowaka moyoni mwako ni kwa ajili ya kukupa onyo ya kuwa kuna jambo lililomkasirisha mungu na lina adhabu inayokuja kama malipo ya kosa hilo na ili ujumbe wa moto huu wa mungu unaokuja kwa jinsi hii yaani uliobeba ghadhabu yake na maonyo yake uwezo kueleweka huwa hauji pekee yake.
Moto wa jinsi hii utawekwa na kudhihirishwa ndani ya moyo wa mtu na Roho Mtakatifu
Roho mtakatifu ataambatanisha moto huu pamoja na hofu ya mungu na huzuni ya mungu na maombolezo na kukunyima amani ya kristo moyoni na au kukukosesha raha nafsini.
Hofu ya mungu inapoambatana na moto wa mungu moyoni mwa mtu ni ujumbe toka kwa Roho Mtakatifu ya kuwa moyo na mtu huyo usije ukadharau onyo hilo la ujio wa ghadhabu ya mungu.
Na unapoona hofu ya mungu ikiwa imeambatana na moto wa mungu unaona pia vimeambatana na huzuni ya mungu na hali ya kuomboleza moyoni au hali ya kukosa amani au hali ya kukosa raha ujue ni roho mtakatifu anakujulisha ya kuwa pamoja na kwamba ghadhabu ya mungu inakuja.
Lakini inawezekana ikaepushwa kwa njia ya mtu kukubali maonyo na kutubu.
Hili tunalipata tunaposoma kitabu cha ( wakorintho 7:10 ) Ya kwamba maana huzuni iliyo kwa jinsi ya mungu hufanya toba liletao wokovu lisilo na majuto.
Hivi ndivyo pendo la mungu linavyofanya kazi, mungu anapoghabika kwa sababu ya kosa la mtu Roho Mtakatifu anampa mtu huyo taarifa ya ghadhabu hiyo lakini pia na onyo ambalo akilitii na kutubu ghadhabu ya mungu inafutwa na kuondolewa.
Fahamu jambo hili ya kuwa Roho Mtakatifu anaweza kumuongoza mtu kwa jinsi hii
____ Kwa ajili ya mtu huyo mwenyewe

___ Au kwa ajili ya mtu mwingine ili apewe hiyo taarifa na kuombewa

____ Au kwa ajili ya eneo kama mji au kijiji au kitongoji au nchi ili liombewe.
Amin

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...