Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SOMO: BIBLIA INAFUNUA UKWELI WA MAMBO Na Wilson Mtishbi

Simulizi la uumbaji ktk kitabu cha mwanzo linasema hivi yehova mungu akamfanya mtu kutoka ktk mavumbi ya inchi na kupuliza ktk mianzi ya pua yake pumzi ya uhai, naye mtu akawa nafsi hai usemi " nafsi hai " unatokana na neno la kiebrania " ne phesh " linalomaanisha kiumbe anayepumua ( mwanzo 2:7 ) Hivyo, Biblia inaonyeaha waziwazi kwamba mwanadamu hakuubwa akiwa na nafsi isiyoweza kufa. Badala yake kila mwanadamu ni " nafsi hai " Hiyo ndiyo sababu hakuna andiko ktk Biblia linalotaja kuhusu "nafsi isiyoweza kufa " Ikiwa Biblia haisemi kwamba wanadamu wana nafsi isiyoweza kufa kama wengine wanavyodai, kwa nini dini nyingi hufundisha jambo tofauti ? Misri ya kale inatoa jibu la swali hilo

JE WANADAMU WANAWEZA KUISHI MILELE
Miaka michache iliyopita, watafiti waliripoti kugunduliwa kwa mimea fulani inayoota chini ya maji wanayoamini imeiahi kwa maelfu ya miaka, huenda muda mrefu kuliko kiumbe kingine chochote duniani. Mimea hiyo ni ya jamii ya posidonia oceanica, aina fulani ya nyasi zilizoenea kwenye sakafu ya bahari ya mediterania kati ya Hispania na saiprasi. Ikiwa mimea inaweza kuishi kwa miaka mingi hivyo namna gani wanadamu ? Baadhi ya wanasayansi ambao huchunguza suala la uzee wanahisi kwamba kuna uwezekano wa kuongeza muda wa kuishi kwa mfano kitabu fulani kuhusu suala la uzee kinasema kuwa kinachunguza kwa kina " Maendeleo makubwa ya kisayansi " ktk nyanja hiyo hatujui ikiwa maendeleo ya kisayansi yatakuwa na mchango wowote ktk kongeza muda wa kuishi wa mwanadamu au la. Hata hivyo, tumaini la kweli la kuishi milele halitegemei sayansi. Biblia inatuelekeza kwa muumba wetu yehova mungu, na kusema hivi " kwako wewe iko chemchemi ya uzima ( zaburi 36: 9 ) Yesu kristo alisali hivi kwa mungu " Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma yesu kristo ( yohana 17: 3 ) Kwa kweli jitihada zetu za kumjua na kumendeza yehova mungu na mwana wake yesu kristo, zitathawabishwa kwa baraka za milele.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...