Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Roho Mtakatifu part 6 Na Mwl Christopher Mwakasege

Roho Mtakatifu Anaweza Kutumia Ukiwa Ili Kukuongoza Ktk Maisha Yako

Unachotakiwa kujua mapema ni kwamba ndani ya Roho Mtakatifu hakuna ukiwa lakini roho mtakatifu anaweza kutumia ukiwa anaoukuta mahali ambapo watu wanakaa au wanapotakiwa kukaa.
Biblia inatueleza na kutufahamisha ktk ( mwanzo 1:1 ) ya kuwa hapo mwanzo mungu aliziumba mbingu na nchi na wakati huo huo mstari unaofuata unatufahamisha ya kuwa nchi ilikuwa ukiwa tena utupu na giza ( mwanzo 1:2 )
Ukisoma mistari hii kwa haraka ni rahisi kufikiri ya kuwa mungu aliumba nchi pamoja na ukiwa na utupu taarifa tofauti.
Tunajifunza ktk somo la leo jinsi Roho Mtakatifu anavyotumia ukiwa kumwongoza mtu na kwa ajili hiyo hebu tusome ( isaya 45: 18 )
Tuone inasemaje juu ya ukiwa. Mstari huu unasema hivi " maana Bwana aliyeziumba asema hivi yeye ni mungu ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya ndiye aliyelifanya imara hakuiumba ukiwa aliumba ili ikaliwe na watu mimi ni Bwana, wala hapana mwingine"
Ni dhahiri ya kwamba mungu hakuiumba dunia iwe ukiwa kwa hiyo hakuiumba nchi pamoja na ukiwa ila mungu aliiumba dunia ikaliwe na watu.
Hii inatupa kujua ya kuwa ukiwa na watu havitakiwi kukaa pamoja palipo na watu hapatakiwi kuwa na ukiwa na palipo na ukiwa hapatakiwi watu kukaa.
Hii ina maana ya kwamba kuna jambo ambalo halijawa wazi juu ya kile kilichotokea kati ya ( mwanzo 1:1 ) ( mwanzo 1:2 ) ikiwa kufuatana ( isaya 45: 18 )
Ukiwa haukuumbwa na mungu ukiwa wa ( mwanzo 1:2 ) ulitoka wapi ( Ezekiel 15:8 ) inatupa jibu la swali hilo mstari huu unasema hivi.
Nami ni taifa kwa sababu wamekosa asema Bwana mungu kosa lililosababisha ukiwa. ( mwanzo 1:2 ) lilifanyika lini na lilifanywa na nani Biblia iko kimya juu ya jambo hili kwa hiyo pamoja na kwamba mungu hakuumba dunia pamoja na ukiwa ( isaya 45: 18 )
Lakini baadaye ( na Biblia haisemi ni lini ) mungu aliifanya nchi kuwa ukiwa ili iwe ishara ya taarifa kwa mwanadamu ya kuwa kuna kosa lililofanyika na kwamba linatakiwa lirekebishwe kabla watu hawajaruhusiwa kuishi au kufanya kitu kwenye hilo eneo
Hii ina maana ya kwamba Roho Mtakatifu akikupa kujua kuwepo kwa hali ya ukiwa ujue anataka ufahamu huu ya kuwa kuna jambo linalohitaji matengenezo ktk ulimwengu wa roho
Ukifuatilia jambo hili kwa makini ktk Biblia utaona ya kwamba ukiwa unaweza ukawa juu ya Eneo au juu ya mtu Binafsi au juu ya kikundi cha watu

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Utengenezaji wa sabuni

1: Utengenezaji wa sabuni za mche     Malighafi: 1: Caustic kg 4 2: Maji lita 10 3: Mafuta lita 20 4: Sodium Silicate Kg 2 5: pafyumu mili lita. 250 __  300 6: Chumvi vijiko 2 vikubwa Sabuni hii unaweza kuogea na kufulia inakuwa nzuri sana. Jinsi ya kutengeneza Loweka Caustic kg 4 kwenye maji ya lita 10 kwa siku 3. Ndani ya siku hizo tatu, utakuwa ukikoroga kila siku asubuhi na jioni kwa dakika 5. Kisha chukua sodium silicate kg2 ikifuatiwa na chumvi vijiko 2 vya chakula na mafuta huku unaendelea kukoroga kwa juhudi. Baada ya hapo weka kwenye maumbo kwa siku 3 __ 5 ili igande vizuri. Asante sana rafiki

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya unga

Sabuni ya unga Malighafi. A. Solphonic lita 1 B. Sodium sulphate kilo 3 C. Optical brightener vijiko 10 vya chakula D. Nausa vijiko 10 vya chakula E. Soda ash kilo 3 F. Pafyumu kijiko 1 cha chakula G. Rangi kijiko 1 cha chakula Jinsi ya kutengeneza Andaa malighafi kwa resho kama ilivyoandikwa hapo juu, Beseni na mwiko, kisha weka kimoja kimoja ukianza na herufi A __ G, huku ukikoroga mseto wako kwa muda wa dakika 15 halafu anika sehemu yenye hewa kivulini hadi ikauke. Hapo sabuni yako ya unga itakuwa tayari, iweke kwenye vifungashio ipeleke aokoni