Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mambo saba usiyojua kuhusu tajiri mpya namba moja duniani ( Jeff Bezos )

Rafiki yangu mmoja aliniandikia jana akitaka kujua huyu Bezos hasa ni nani na amewezaje kumpiku mtu tajiri duniani Bill Gates.
Hapa ndipi niligundua wapo wengi hawajawahi kumsikia au kumjua kwa undani Jeff Bezos
Nimekuandalia makala hii yenye mambo saba muhimu ambayo huenda huyajui kuhusu tajiri huyu mpya namba moja duniani yapo mengi ya kujidunza kupitia maisha yake .

1: utoto wake ulikuwa na changamoto:
Mama yake mzazi alipata mimba akiwa shuleni. Baadaye aliolewa na aliyempa mimba lakini waliachana kutokana na maisha kuwa magumu na mwanaume kuwa mlevi.
Baadaye aliolewa na mwanaume mwingine ambaye alimchukulia jeff kama mtoto wake wa kumzaa. Mpaka anafikisha miaka 10

2: Biashara yake kuu ni Amazon
Bezos ni mwanzilishi wa mtandao mkubwa wa kuuza vitu wa Amazon. Ni mtandao ambao ulianza kwa kuuza vitabu, ila kwa sasa unauza kila kitu mtandao huu ulianza tangu mwaka 1994 na umekuwa unakua kwa kasi kubwa kila mwaka.
Kampuni hii alianzia nyumbani kwake alipokuwa anaishi.

3: Amewahi kuwa mhudumu wa mgahawa:
Hakiwa kijana mdogo, Bezos amewahi kuwa mhudumu wa mgahawa wa mc Donald's akiwa kama mhudumu na msafishaji wa meza.
Anasema kazi hii ilimpamsingi muhimu sawa wa kubeba majukumu yake.

4: Aliacha kazi inayolipa kwenda kujijiri

__ Kabla ya kuanzisha Amazon, Bezos alikuwa ameshaajiriwa sehemu tatu, Firel, Bankers Trust company na D.E shaw, zote zikiwa kampuni zinazo hususika na fedha na uwekezaji. Ktk kampuni ya tatu, aliweza kupanda vyeo mpaka kufikia nafasi ya makamu wa rais wa kampuni hiyo, tena ktk umri mdogo sana.
Wakati anaacha kazi yake na kwenda kujiajiri, kila mtu alimwambia anafanya kosa kubwa ambalo atajutia maisha yake yote

5: wakati anaanzisha Amazon hakuwa na uhakika wa anafanya nini
Kabla ya kampuni yake kuitwa Amazon, aliita cadabra, baadaye akaona halifai Baadaye ndiyo aliamua kuchagua Amazon, jina la mto mrefu zaidi akiwa na maono ya kampuni kuwa kubwa zaidi.

6: Amewekeza kwenye makampuni mengine zaidi ya 40
Bezos amekuwa mwekezaji mkubwa kwenye makampuni mengine kama google, Twitter, uber nk Alikuwa mwekezaji wa kwanza kabisa kuwekeza kwenye kampuni ya google kabla hata haijajulikana,aliwekeza dola 250, 000 mwaka 1998.
Wakati huo hisa moja ya google ilikuwa dola 0.04.
Sasa hivi hisa moja ya google inathamani ya dola 966.
Hii ina maana kama hakuuza hisa zake dola laki mbili na nusu aliyowekeza mwaka 1998, sasa hivi imefikia dola bilion sita

7: Anampango wa kuwaondoa binadamu duniani
Lakini siyo kwa kuwaangamiza, bali kwa kuwawezesha kuishi kwenye sayari nyingine .
Kupitia kampuni yake ya Blue origin aliyoianzisha mwaka 2000, anataka watu kwenda sayari nyingine iwe rahisi na nafuu kama watu wanavyosafiri kwenda nchi nyingine

NYONGEZA: Nafasi Bezos kuwa tajiri namba moja duniani ili dumu kwa muda mfupi baada ya thamani za hisa zake kushuka. Hii ili pelekea kuwa mtu tajiri namba mbili duniani,namba moja akiwa Bill Gatess.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...