Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kwa nini mungu Aliumba dunia Na Wilson Mtishbi

Yehova aliwapa wanadamu dunia. Dunia ni makao yetu. Kwa hiyo wanadamu wa kwanza, Adamu na hawa, hawakuumbwa waijaze mbingu kwa kuwa tayari mungu alikuwa amewaumba malaika waishi mbinguni ( ayubu 38:4,7 ) Badala yake mungu alimweka mwanadamu wa kwanza ktk paradiso yenye kupendeza iliyoitwa bustani ya Edeni ( mwanzo 2:15,17 ) yehova alimpa adamu na watoto ambao angepata tumaini la kufurahia maisha duniani milele ( zaburi 37:29, 115:16 ) mwanzoni, bustani ya Edeni tu ndiyo iliyokuwa paradiso wanadamu hao wa kwanza walipaswa kuzaa na kuijaza dunia.
Baada ya muda, wangeitiisha dunia nzima na kuifanya kuwa paradiso ( mwanzo 1:28 ) dunia haitaharibiwa kamwe.

Kwa nini dunia si paradiso leo
Adamu na hawa hawakumtii mingu, hivyo yehova akawafukuza kutoka ktk bustani hiyo. Paradiso ikapotea na hakuna mtu ambaye amefanikiwa kuirudisha.
Biblia inasema dunia imetiwa mkononi mwamwovu ( ayubu 9:24 ) ( mwanzo 3:23,24 )
Je, yehova ameshindwa kutimiza kusudi lake la awali kuelekea wanadamu hapana yeye ni mweza yote hawezi kushindwa ( isaya 45: 18 ) Atawarudisha wanadamu ktk hali ambayo alikusudia wawe nayo ( zaburi 37:11:34 )

Paradiso itarudishwa jinsi gani
Paradiso itarusishwa duniani yesu atakapotawala akiwa mfalme aliyewekwa na mungu.
Ktk vita vinavyoitwa Har magedoni, yesu atawaongoza malaika wa mungu kuwaharibu wote wanaompinga mungu kisha yesu atamfunga shetani kwa miaka 1000.
Watu wa mungu wataokoka uharibifu huo kwa sababu yesu atawalinda na kuwaongoza.
Watafurahi uzima wa milele ktk paradiso duniani ( ufunuo 20:1,3, 21: 3,4 )

Kuteseka kutaisha lini
Mungu ataondoa uovu dunia lini ??
yesu alitoa ishara ya kuonyesha wakati ambapo mwisho ungekuwa karibu.
Hali zilizo ulimwenguni leo zinahatarisha maisha ya watu na zinaonyeaha kwamba tunaishi katika umalizio wa mfumo wa mambo ( mathayo 24:3,7 ) ( 14:21,22 )
Wakati wa utawala wa miaka 1,000 wa yesu atakapo kuwa akiitawala dunia kutoka mbinguni, atakomeaha kuteseka kote ( isaya 9:6, ( isaya 7:11,9 ) zaidi ya kutawala akiwa mfalme yesu atatenda akiwa kuhani mkuu naye atazifuta dhambi za wale wanaompenda mungu hivyo, kupitia yesu, mungu ataondoa magonjwa, uzee na kifo ( isaya 25: 8 ) ( isaya 33: 24 )

Ni nani watakaoishi ktk paradiso
Ktk jumba la ufalme, utakutana na watu wanao mpenda mungu na wanaotaka kujifunza jinsi wanavyo weza kumpendeza watu wanaomtii mungu wataishi katika Paradiso ( 1yohana 2:17 ) yesu aliwatuma wafuasi wake wawatafute watu wapone na kufundisha jinsi ya kuwa watu wenye kukubalika mbele za mungu.
Leo yehova anawatayarisha mamilioni ya watu kuishi ktk paradiso ijayo hapa duniani ( sefania 2:3 ) ( mika 4:1,4 ) amin

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...