Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kilimo cha nyanya; maandalizi ya mbegu, shamba na upandaji wa miche

Uzalishaji wa nyanya duniani na hapa Tanzania nchi zinazolima nyanya kwa wingi duniani ni pamoja na USA, Italia na Mexico.
Kwa upande wa Afrika nchi zinazo lima ni kama malawi, Zimbia na Botswana.
Zao hili hulimwa pia katika nchi za afrika mashariki ikiwemo kenya,uganda na tanzania.
Zao la nyanya linalimwa karibu maeneo yote ya Tanzania.
Uzalishaji wa nyanya ni mkubwa kuliko mazao mengine ya mbogamboga yanayolimwa hapa Tanzania, uzalishaji wa nyanya kwa mwaka ni jumla ya tani 129,578 Ikiwakilisha asilimia 51 ya mazao yote ya mboga.
Kwa mujibu wa wizara ya kilimo ya tanzania maeneo yanalolima sana nyanya ni pamoja na mkoa wa kilimanjaro ( Hai, moshi na Rombo ) Arusha ( Arumeru ) Morogoro ( Mgeta ) Tanga ( Lushoto ) Mbeya ( Mbeya Vijijini ) na Singida.
Morogoro ndiyo inayoongoza kwa kilimo hichi ikiwa na wazalishaji wenye zaidi ya hekta 6,159 ( ekari 15, 398 ) pamoja na kwamba eneo la uzalishaji wa nyanya bado ni mdogo sana.
Uzalishaji mdogo unasababishwa na kupungua kwa rutuba ya ardhi, Upepo, Joto, Ukame.

Aina za nyanya

Kutokana na tabia ya ukuaji, nyanya zinagawanyika ktk makundi mawili.

a: Aina ndefu ( inter mediate ) kwa mfano ANNA FI, Tebgeru 97. Aina hizi hufanya vizuri zaidi zinapopandwa ndani ya green house.
Uvunaji wake ni wa muda mrefu, Zipo ambazo zinavunwa hata zaidi ya miezi 6, yaani hiyo miezi 6 ni ya uvunaji.

b: Aina fupi ( determinate ) kwa mfano Tanya, cal, mwaga, onyx, Roma VF ( nyanya mshumaa ) kutokana na uchavushaji, nyanya zinagawanyika makundi

1: OPV ( open pollinated Variety ) Aina za kawaida

2: Hybrid - chotara: Hizi ni aina zenye mavuno mengi, kati ya hizo zipo aina fupi na ndefu.
Katika karne hii ya 21, nyanya zinazopendelewa kulimwa zaidi na wakulima l, ni zile zinazoweza kuvumilia magonjwa, zinazo zaa sana na zanye ganda gumu ili kufanikisha usafirishaji, na kuhifadhika kwa siku nyingi bila kuharibika mapema.

Kuandaa kitalu cha nyanya mambo muhimu ya kuzingatia

__  Kitalu kiwe karibu na maji ya kutosha na ya kudumu

__ Kiwe sehemu iliyowazi na yenye udongo ulio na rutuba ya kutosha

__ Eneo la kitalu kama ni kubwa liwe tambarare au na mwiinuko kidogo ili kuepuka maji yasituame kwenye kitalu, mtelemko ukiwa mkali sana nao sio mzuri kwani husababisha mmonyoka wa udongo

__ Kitalu kiwe sehemu ambayo haikuwa na zao la nyanya au viazi mviringo ( au mazao ya jamii ya nyanya k.m. mnavu, biringanya n.k )

__ Kiwe sehemu ambayo ni urahisi, ikiwa ni pamoja na uhamishaji wa miche kwenda sehemu nyingine. Pia kurahisisha usambazaji wa miche kwenda sehemu nyingine

Kuandaa matuta ya kusia mbegu za nyanya Aina ya matuta:

__ Matuta ya makingo ( sunken seed bed )

__ Matuta ya kunyanyulia udongo ( raised seed bed )

__ Matuta ya kawaida ( flat seed beds )

Mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa kuandaa matuta

. Tuta liwe na upana kati ya sentimita 90-120, na urefu wowote, [ Ili mradi muhudumu anaweza kutoa huduma nyingine zote kitaluni bila kukanyanga miche ]

. Kwatua / lima kina kirefu cha kutosha kiasi cha sentimita 15-20 ili mizizi iweze kusambaa vizuri ardhini

. Choma takataka juu ya kitalu, au funika tuta kwa nailoni, majuma 4-8 ili kuua vimelea vya magonjwa na wadudu

. Wakati wa kuandaa, kitalu, ongeza mbolea aina ya samadi/ vunde au mboji kwenye udongo kisha kwatua ili ichanganyike vinzuri na udongo

. Changanya kiasi cha debe 1 hadi 2 kila baada ya mita moja ( hatua moja ) mraba

. Tuta lisiwe na mabonde mabonde mabonde au mawemawe ambacho yanaweza kuzuia usambaaji mzuri wa mbegu kwenye tuta, lisawazishwe.

Faida na hasara za matuta yaliyotajwa hapo juu

1 Matuta ya kunyanyulia udongo ( raised seed beds )

__ Matuta ya namna hii huruhusu maji, hewa na mizizi kupenya kwenye udongo kwa urahisi zaidi.

__ Mazao ya mizizi hupata nafasi ya kutoaha kutanuka haraka zaidi

__ Matuta haya hayatuamisho maji kama mengine. Hivyo hutumika zaidi kwenye maeneo yanayokuwa na mvua mara kwa mara

Hasara
Matuta ya namna hii yana sababisha sana mmomonyoko wa udongo kama haya kutengenezwa vinzuri.

2: matuta ya makingo ( sunken seed beds ) faida:
__ Matuta haya ni raisi kutengeneza

__ Hutumika wakati wa kiangazi ili kuhifadhi maji na unyevu

__ Nyevu mdogo unaopatikana ardhini

__ Ni rahisi kumwagilia kwa kutumia maji ya mfereji au bomba

__ Huhifadhi unyevu nyevu kwenye ardhi kwa muda mrefu

__ Huzuia mmonyoko wa ardhi

Hasara
Matuta ya aina hii hayanawezi kutumika kwenye maeneo yenye mvua nyingi.

3: matuta ya kawaida ( Flat seed beds )

Faida

__ Ni rahisi sana kutengeneza kwani udongo ukisha kwatuliwa na kusambazwa mbegu huoteshwa

__ Ni rahisi kutumia eneo kubwa kuotesha mbegu

Hasara
Matuta ya aina hii hayawezi kutumika kwenye maeneo yenye mvua nyingi

Kusia mbegu
__ Hakikisha ubora na uotaji wa mbegu kabla ya kuzipanda kitaluni ( Germination test )

__ Weka mistari kwenye tuta kulingana na ukubwa wa tuta, lakini mistari isiwe chini au zaidi ya sentimita 15-20 toka mstari hadi mstari

Asante sana kwa kusoma nakala hii Tuta endelea wakati mwingine "ASANTE SANA"

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...