Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kanuni saba za upatanisho ktk mahusiano


Tofauti ktk mahusiano ni jambo ambalo halikwepeki na hakuna mahusiano yasiyo kuwa na tofauti

Pindi watu waliokatika mahusiano wanapotofautiana ni bora wakazijua kanuni hizi

1: watambue neno SAMAHANI halina jinsi Aliyekosea ndiye aombe kusamehewa hili halijalishi ni mme au mke ubabe ktk mahusiano si njia bora ya kumaliza tofauti zenu

2: Tabia ya kususa susa siyo nzuri wengine wakisha tofautiana hususa wakidhani ndio wanatatua tofauti zao wengine hususa kuongeza wengine hususa kula na mbaya zaidi

3: Ugomvi unaoanzia chumbani uishie chumbani huko huko ma usitoke nje. Walio ktk mahusiano wajitahidi kusikiliza na kutatua tofauti zao wenyewe na zaidi kitandani kiwe jukwaa la upatanishi na siyo vinginevyo

4: Mmoja lazima akubali kuumia ili mwenzie apate amani

__  Jifunze kushuka ( some times caln down ) hii itakusaidia kurejesha amani ktk mahusiano yako usipandishe sauti wakati unamwona mwenzio naye yuko juu na kajawa na hasira, kwa kujishusha amani itarejea tu.

5: Acha mawazo ya kuachika
Huyo mi wako zaidi waza urejesho na siyo uharibifu. Mkubaliane mkapatana na mkayaanzisha mahusiano. Usivunje mahusiano uliyoyajenga kwa muda na gharama kubwa kwa jambo dogo sana. Talaka haijawahi kumwacha mtu salamaa.

6: Samehe
Achilia na mchukulie mwenzio hakuna aliye mkamilifu ktk dunia hii. Sisi wote tuna madhaifu ( weekness ) unapoona mahusiano yamedumu ujue hao wamefuzu kiwango cha juu. Kuvumiliana na kuchukuliana

7: Jenga utaratibu wa kufanya ibada pamoja

__  Sote tunajua mpatanishi mkuu ni mwenyenzi mungu. Hivyo mnapounganisha mikono yenu kwa pamoja na mkamuita mungu awasaidie hakika mtakuwa sehemu salama kuliko ukifanya vinginevyo mahusiano yanayotegemea mungu huwa hayateteleki.

Asante sana.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya vyoo

Sabuni ya kusafisha vyoo Malighafi. 1. Sulphonics Acid Lita 1 2. Soda Ash nusu 1/2 kilo 3. Sless 4. Chumvi 1/2 kilo 5. Maji lita 17 1/2 _ 20 6. Rangi kijani 7. Pafyumu 8. Formalin Jinsi ya kutengeneza Weka maji lita 5 kisha anza kukoroga, ongeza lita 5 kisha lita 5 tena na mwisho lita 2 4. Chumvi 1/2 kg 3. Sless nusu lita 2. Soda ash nusu kilo 1. Sulphonics Acid lita 1 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu ni vinzuri kuweka kwenye ndoo lita 10 ya sabuni utaweka rangi kijiko 1 cha chai, rangi ya kijani pafyumu aina ya ' Rose two one ' au pino vijiko 5 vya chakula na Formalin vijiko 3 vya chakula. Formalin kwa ajili ya kuua wadudu ( bacteria ) ni vinzuri sana kuwemo kwenye sabuni ya chooni kwani ina kazi nyingi zaidi ya hiyo iliyotajwa Asante sana rafiki sasa chukua hatua ya kufanya hakika utafanikiwa sana

Somo: Roho mtakatifu Na mwl Christopher Mwakasege

Kushirikiana Na Roho Mtakatifu Anapotumia Moto kukuongoza ili utembee kwenye mapenzi ya mungu Biblia inafundisha ya kuwa wana wa mungu huwa wanaishi na wanatakiwa waishi kwa kuongozwa na roho mtakatifu ( warumi 8 : 14, 16, 17 ) Njia moja wapo anayotumia roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa mungu, ni kwa kutumia moto wa mungu anaokuja nao ndani ya mtu anapoingia kukaa kwake Biblia inasema juu ya yesu ya kuwa yeye atawabatiza kwa roho mtakatifu na kwa moto ( luka 3 : 16 ) na siku ya pentekoste, wakati wanafunzi wa kwanza wa yesu, walipokuwa wamekutanika pamoja kukuwatokea ndimi zilizogawanyika, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao wote wakajazwa roho mtakatifu ( matendo 2 : 3,4 ) Unaposoma na kutafakari jambo lililotokea siku hiyo ya pentekoste, utajua kuwa kuna uhusiano kati ya ndimi za moto juu ya kila mmoja wao na kule kujazwa roho mtakatifu kwa kila mmoja wao ni dhahiri ya kuwa roho mtakatifu anaingia ndani ya kila mwana wa mungu akiwa pia na moto wa mungu pamoja nao kazi m...