Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ELEMENTI YA AJABU Na Wilson mtiahbi

"Hakuna elementi iliyo muhimu zaidi ktk uhai kama kaboni," Kinaeleze kitabu Nature's Building Blocks. Muundo wa kaboni huiwezesha kuungana yenyewe na pia na kemikali nyingine nyingi, hivyo kufanyiza mamilioni ya miungano tata, na mingi kati ya miungano hiyo bado haijagunduliwa au kujulikana. Mifano ifuatayo inaonyeasha, jinsi atomu za kaboni zinavyoweza kuungana na kutokeza maumbo ya aina mbalimbali, kama vile minyororo, piramidi, pete, mabamba, na mirija. Kwa kweli, kaboni ni elementi ya ajabu
Kaboni___ Elementi inayotokana na Utendaji wa Nyota
Kaboni hutokana na miungano ya viini vitatu vya heliamu, ambavyo wanasayansi huamini kwamba vinapatikana ktk nyota kubwa ziitwazo majitu mekundu. Hata hivyo, ili heliamu ziungane, lazima hali fulani itokee kwa usahihi kabisa. Mwanafizikia Paul Davies alindika hivi: " Kubadili mambo machache tu [ katika sheria za asili ] Hata kwa kiasi kidogo sana, kungefanya kusiwepo ulimwengu, Uhai, Hata wanadamu." Tunajua jinsi gani kwamba hali hiyo hujitokeza yenyewe tu. Wengine huamini kwamba huo ni uthibitisho wa kuwapo kwa muumba mwenye hekima. Unafikiri ni maoni gani yaliyo sahihi?

ALMASI : Atomu za kaboni zinapoungana hutakeza piramidi ziitwazo tetrahedron, zilizo na umbo imara na hufanya almasi kiasili iwengumu kuliko kitu chochote. Kimsingi almasi halisi ni molekuli iliyofanuizwa na atomu za kaboni

GRAFITI : Ni tabak la atomu za kaboni zilizoungana na kujipanga kwa kuachiana nafasi kwa njia inayoweza kupekuliwa kama kurasa za kitabu. Kwa hiyo grafiti ni laini na ni muhimu katika utengezaji wa penseli. Ni tabaka moja la atomu za kaboni lenye mpangilio wenye matundu yenye umbo la penseli inaweza kuwa na kiasi kidogo cha grafati katika tabaka moja au zaidi

MOLEKULI ZA FULLERENE : Hizi ni molekuli za kaboni zenye mashimo na umbo la mviringo kama mpira na zingine zenye umbo la mirija zinazoitwa nanotube. Hupimwa katika nanometa, au mabilioni ya meta.

VIUMBE HAI : Chembe nyingi zinazofanuiza mimea, wanyama, na mwanadamu zinatokana na kaboni, yaani, elementi inayopatikana katika kabohaidreti, mafuta, na aminoasidi.
    
" Sifa za [ Mungu ] ambazo hazionekani.. Zinaeleweka kwa vitu vilivyofanywa." __ warumi 1: 20 inasema hivi " kwa sababu mambo yake yasiyoonekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake; yaani, uweza wake wa milele na uungu wake; hata wasiwe na udhuru

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Utengenezaji wa sabuni

1: Utengenezaji wa sabuni za mche     Malighafi: 1: Caustic kg 4 2: Maji lita 10 3: Mafuta lita 20 4: Sodium Silicate Kg 2 5: pafyumu mili lita. 250 __  300 6: Chumvi vijiko 2 vikubwa Sabuni hii unaweza kuogea na kufulia inakuwa nzuri sana. Jinsi ya kutengeneza Loweka Caustic kg 4 kwenye maji ya lita 10 kwa siku 3. Ndani ya siku hizo tatu, utakuwa ukikoroga kila siku asubuhi na jioni kwa dakika 5. Kisha chukua sodium silicate kg2 ikifuatiwa na chumvi vijiko 2 vya chakula na mafuta huku unaendelea kukoroga kwa juhudi. Baada ya hapo weka kwenye maumbo kwa siku 3 __ 5 ili igande vizuri. Asante sana rafiki

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya unga

Sabuni ya unga Malighafi. A. Solphonic lita 1 B. Sodium sulphate kilo 3 C. Optical brightener vijiko 10 vya chakula D. Nausa vijiko 10 vya chakula E. Soda ash kilo 3 F. Pafyumu kijiko 1 cha chakula G. Rangi kijiko 1 cha chakula Jinsi ya kutengeneza Andaa malighafi kwa resho kama ilivyoandikwa hapo juu, Beseni na mwiko, kisha weka kimoja kimoja ukianza na herufi A __ G, huku ukikoroga mseto wako kwa muda wa dakika 15 halafu anika sehemu yenye hewa kivulini hadi ikauke. Hapo sabuni yako ya unga itakuwa tayari, iweke kwenye vifungashio ipeleke aokoni