Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Biblia inasema nini mwisho wa dunia utkuja lini Na Wilson Mtishbi

Mwisho utakuja wakati wanadamu watakapokuwa wameonywa kikamili kupitia kazi ya ulimwenguni pote ya kutangaza ufalme wa mungu. Ufalme huo ni serikali itakayotawala dunia nzima wakati ambapo serikali za wanadamu zitaondolewa ( daniel 7:13,14 ) yesu kristo alisema hivi " hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote na inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote na ndipo ule mwisho utakapokuja ( mathayo 24:14 ) kazi hiyo ya kuhubiri, inayoonyesha haki na rehema ya mungu ni sehemu ya ishara yenye mambo mengi ya siku za mwisho ishara hiyo inatia ndani pia vita kati ya mataifa matetemeko ya inchi, njaa, na magonjwa ( mathayo 24:3 ) ( luka 21:10,11 ) mbali na kutabiri matukio ya ulimwengu Biblia inatueleza pia kuhusu mabadiliko ya kijamii katika siku za mwisho inasema hivi kutakuwa na nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe wenye kupenda pesa wasiotii wazazi wasiojizuia, wakali, wasiopenda wema, wanaopenda raha badala ya kumpenda mungu ( 2 Timotheo 3:1,5 ) ulimwengu huu mwovu karibuni utapitilia mbali ( 1 yohana 2:17 ) hali hizo zina tambulisha kipindi kilichoanza mwaka 1914 hivi, wakati wa vita vya kwanza vya ulimwengu.
" kwa hiyo, endeleeni kukesha kwa sababu hamwijui ile siku wala saa " ( mathayo 25 :13 )

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji

Jinsi ya kutengeneza sabuni ya maji Malighafi: 1. Sulphonic Acid Lt 2 2. Soda Ash Kg 1 3. Sless Lt 1 4. Chumvi Kg 1 5. Pafyumu /rangi Bluu 6. Maji Lt 35 _ 40 Jinsi ya kutangeneza Anza kwa kuweka lita 10 mara tatu, yaani lita 10 tena na mwisho lita 10, angalia uzito ongeza tena lita 5 na kisha lita 2 ikiwa uzito bado ongeza lita 2 na mwisho lita 1 4. Chumvi kg 1 3. Sless Lt 1 2. Soda Ash Kg1 1. Sulphonics Acid Lt 2 Hapo sijaweka rangi wala pafyumu kwa sababu ukiweka pafyumu lita 35 bila kufunika itaisha baada ya muda mfupi. Ni vema rangi na pafyumu uweke pembeni. Mfano: Chukua ndoo ya lita 10, weka rangi robo kijiko cha chai na pafyumu vijiko vya chakula viwili na koroga vizuri. Ni vema utumie pafyumu aina ya lemon. Sababu za kutoweka rangi sabuni yote: Wapo wateja hawapendi rangi na harufu kwa hiyo utawapa kila mtu kama atakavyo na kujaza kwenye chupa zako zenye mifuniko saa hiyo hiyo ukiachia muda inatoka harufu. Asante sana rafiki.

Utengenezaji wa sabuni

1: Utengenezaji wa sabuni za mche     Malighafi: 1: Caustic kg 4 2: Maji lita 10 3: Mafuta lita 20 4: Sodium Silicate Kg 2 5: pafyumu mili lita. 250 __  300 6: Chumvi vijiko 2 vikubwa Sabuni hii unaweza kuogea na kufulia inakuwa nzuri sana. Jinsi ya kutengeneza Loweka Caustic kg 4 kwenye maji ya lita 10 kwa siku 3. Ndani ya siku hizo tatu, utakuwa ukikoroga kila siku asubuhi na jioni kwa dakika 5. Kisha chukua sodium silicate kg2 ikifuatiwa na chumvi vijiko 2 vya chakula na mafuta huku unaendelea kukoroga kwa juhudi. Baada ya hapo weka kwenye maumbo kwa siku 3 __ 5 ili igande vizuri. Asante sana rafiki

Fahamu jinsi ya kutengeneza sabuni ya unga

Sabuni ya unga Malighafi. A. Solphonic lita 1 B. Sodium sulphate kilo 3 C. Optical brightener vijiko 10 vya chakula D. Nausa vijiko 10 vya chakula E. Soda ash kilo 3 F. Pafyumu kijiko 1 cha chakula G. Rangi kijiko 1 cha chakula Jinsi ya kutengeneza Andaa malighafi kwa resho kama ilivyoandikwa hapo juu, Beseni na mwiko, kisha weka kimoja kimoja ukianza na herufi A __ G, huku ukikoroga mseto wako kwa muda wa dakika 15 halafu anika sehemu yenye hewa kivulini hadi ikauke. Hapo sabuni yako ya unga itakuwa tayari, iweke kwenye vifungashio ipeleke aokoni